Search This Blog

Tuesday, June 25, 2013

WABUNGE WAFANYA JOGING MKOANI DODOMA

 Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan akiwapanga washiriki wa Joging katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia wa pili kutoka (Kulia), Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla wa pili kutoka (kushoto), Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (kulia) na Mbunge wa Kinondoni Idd Azan (kushoto) wakiongoza  mazoezi ya kukimbia ya Kilomita kumi yaliyoanzia katika Uwanja wa Jamhuri  na kushirikisha baadhi ya wabunge, timu ya Barafu Joging ya Dar es Salaam na Muungano ya mkoani Dodoma.
 Hawa Ghasia na Idd Azan wakishiriki Joging mkoani Dodoma leo

 washiriki wa Joging timu ya muungano kutoka mkoani Dodoma na timu ya Barafu Joging Sports Club ya jijini Dar es Salaam wakiwa pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia
washiriki wa Joging wakifanya mazoezi ya viungo baada ya kumaliza mbio za kilomita kumi
 Hawa Ghasia akiwa na timu ya Joging ya Barafu Sports Club na Muungano
 Kulia ni Mbunge wa Nzega Dk. Khamis Kigwangala akishiriki mazoezi ya viungo baada ya kumaliza mbio za kilomita kumi


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia akishiriki mazoezi ya viungo
Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa akishiriki Joging katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma

1 comment:

  1. Shaffih kweliwabunge wetu wanaonekana kuwa na ari kubwa michezoni. Cha ajabu wakiwa ndani ya mjengo duh ni maji na mafuta

    ReplyDelete