Search This Blog

Friday, June 28, 2013

FALCAO, MOUTINHO NA WENZAO KUANZA LIGI YA UFARANSA WAKIWA NA PENGO LA POINTI 2 - VURUGU ZA MASHABIKI ZAWAPONZA


Monaco tayari wameshatumia kiasi kisichopungua €120 million kama ada ya uhamisho kwa wachezaji wake wampya wakijiandaa na msimu ujao wa  Ligue 1, lakini mapesa yao yote hayotoweza kuwazuia kuanza ligi wakiwa nyuma ya timu zote kwenye ligi kwa pointi 2. Tukio lilotokea wakati wa mchezo wao wa mwisho wa Ligue 2 ambao walishinda ubingwa wa ligi hiyo na kupanda daraja, ambapo kulitokea vurugu uwanjani limesababisha kukatwa pointi 3 (moja imewekwa pembeni, hivyo inamaanisha kwamba itaongezwa kwenye adhabu ikiwa kutatokea tukio la namna hiyo tena.

Kutoka Reuters:
Kuliwashwa moto wakati wa mechi ya mwisho ya ligue 2 Monaco wakicheza kwenye uwanja wao wa nyumbani dhidi ya Le Mans, kabla ya mshabiki hawajavamia uwanjani baada ya filimbi ya mwisho. Refa aliumizwa na mashabiki kwa mujibu wa ripoti ya kamisaa wa mchzo huo.
"Kwa tukio hilo, Monaco watacheza mechi moja bila uwepo wa mashabiki na pia wamekatwa pointi 3 watakapoanza kucheza kwenye ligue 1 msimu ujao," ilisema taarifa ya shirikisho la soka la Ufaransa LFP .

No comments:

Post a Comment