Search This Blog

Friday, June 28, 2013

COASTAL UNION WAENDELEZA BALAA KWENYE USAJILI - WAMSAJILI MKENYA ALIYEWAHI KUKIPIGA AZAM, KUUNDA SAFU YA KIUNGO NA BOBAN PAMOJA NA SANTO


Klabu ya Coastal Union imeendeleza harakati za kukijenga vyema kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom kwa kumsajili mchezaji wa kimataifa wa Kenya Crispin Odula kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Bandari ya nchini Kenya.

Crispin Odula ambaye aliwahi kuicheza Azam FC huko nyuma, amesajiliwa baada ya kocha Hemedy Morocco kutoa maagizo kwa uongozi kwamba kiungo huyo wa kikenya anahitajika kwenye timu yake. Akiwa na malengo ya kumtumia Odula, Jerry Santo na Haruna Moshi Boban katika kuunda safu imara ya kiungo ya timu hiyo.

Mkurugenzi wa ufundi wa Wagosi wa Kaya Nassor Ahmed 'Binslum' mwenye kofia akiwa na kiungo mshambuliaji kutoka Bandari ya Mombasa aliyesaini kuungana na kikosi cha Coastal Union CRISTIN ODULA (katikati), kulia ni mwakilishi wa Coastal Union jijini Mombasa Kenya ndugu Hussein Tawakkal.

No comments:

Post a Comment