Search This Blog

Thursday, June 20, 2013

BRAZIL WATENGENEZA REKODI MBILI TOFAUTI JANA BAADA YA KUITWANGA MEXICO - DE ROSSI NAE AINGIA KWENYE VITABU VYA REKODI VYA KOMBE LA MABARA


Baada ya michezo ya jana ya kombe mabara leo tunakuletea takwimu na rekodi zilizotengenezwa jana.

 - Brazil ilitengeneza rekodi mbili jana kwenye kombe la mabara kwa ushindi wao dhidi ya Mexico. Ulikuwa ushindi wao wa tisa mfululizo na mechi yao ya 10 bila kufungwa. 

 - Mexico sasa wameruhusu nyavu zao kuguswa mara 32 kwenye kombe la mabara, mabao mengi kuliko timu yoyote.  


 
- Daniele De Rossi ndio muitaliano wa kwanza kufunga katika michuano miwili ya kombe la mabara - mara ya kwanza alifunga mwaka 2009 - dhidi ya USA.

 - Timu pekee ambayo iliwahi kutoka nyuma kwa 2-0 na kwenda kushinda katika kombe la mabara ilikuwa ni Brazil, ambao walishinda 3-2 katika fainali za mwaka 2009 - walikuwa nyuma kwa mabao mawili.

No comments:

Post a Comment