Search This Blog

Wednesday, May 29, 2013

MAMBO MATATU MUHIMU DAVID MOYES ANAPASWA KUWA AMEFANYA KABLA YA AUGUST NDANI YA MANCHESTER UNITED


Mpaka kufikia mwezi wa nane katikati David Moyes atakumbana na presha kubwa kuliko watu wengi kwenye ulimwengu wa soka. Nani ataweza kumlaumu kwa hili?
Kuvaa viatu vikubwa vya kocha aliye na mafanikio zaidi kwenye soka la Uingereza sio jambo rahisi hata kidogo na kwa bahati mbaya pamoja na Sir Alex Ferguson kuwaomba mashabiki kumpa muda na sapoti Moyes wakati akiwaaga - ukweli ni kwamba ikiwa matokeo hayatokuwa yakiwafurahisha mashabiki mpaka kufikia November, maswali yataanza kuzuka kama mscotland huyo ni mtu sahihi kurithi mikoba ya Fergie?
Pamoja na hilo pia Moyes ana changamoto nyingine kubwa 3 na muhimu za kukabilina nazo kabla ya msimu haujaanza. 

1 - KUHAKIKISHA WACHEZAJI WAKONGWE WOTE WANAMUUNGA MKONO. 

Kama ilivyo kwa vilabu vingi vikubwa basi Manchester United nayo ina wachezaji ambao wanasikilizwa sana ndani ya timu (mafaza); Ryan Giggs, Nemanja Vidic, Rio Ferdinand na Patrice Evra. Baada ya kumalizika kwa siku ya kwanza mazoezini itampasa kuwa na mikutano tofauti na wachezaji hawa, hasa Ryan Gigg. Kujadili mipango yake kwenye timu na wachezaji hawa husika. Chumba cha kubadilishia nguo cha United kina umuhimu mkubwa katika mafanikio katika soka la kisasa kama ambavyo tumeshuhudia Manchester City, Mancini alipoteza sapoti kutoka kwenye 'dressing room' jambo ambalo lilipelekea au kuchangia kufeli kwa City na hivyo kupelekea kutimuliwa kwake. Moyes akifanikiwa kuwaweka mafaza wa United upande wake basi timu itakuwa na umoja mkubwa na hivyo kujirahisishia kazi yake ndani ya Old Trafford.

2 - KUSHUGHULIKIA SUALA LA ROONEY. 

Kitu kimoja ambacho kilimfanya Ferguson awe tofauti na makocha wengine kilikuwa ni kuuza wachezaji kwenye muda sahihi. Sasa hivi kuna suala la mmoja wa wachezaji wa United Wayne Rooney ambaye ameonekana kutaka kuondoka kwenye klabu hiyo kwa mujibu wa Ferguson. Mashabiki wa Manchester United wamegawanyika wengine wakitaka auzwe na wengine wakitaka abaki, mchezaji mwenye ubora wa aina yake inabidi abaki kwa gharama yoyote ni mawazo ya baadhi huku wengine wakidhani kwamba dau la 30+ million kwa Rooney ni biashara nzuri na inaweza ikatoa nafasi kwa wachezaji wachanga kuonekana, wachezaji wenye njaa ya mafanikio wenye kucheza nafasi ya Rooney.
Imeanza kuwa hali kama iliyojitokeza wakati wa David Beckham, Rooney ameanza kuhisi amekuwa mkubwa kuizidi klabu ya Manchester United, kukasirishwa na kutopata muda mwingi wa kucheza katika mechi alizokuwa fiti, akiwa tayari ameshaomba kuuzwa inaonekana uhusiano baina ya Rooney na Manchester United upo kwenye hali mbaya. Moyes anahitaji kumuuliza Rooney kama anahitaji kuendelea kuichezea Manchester United, kama hahitaji itabidi amuuze kwa dili zuri na kumbadili na mchezaji sahihi, kama Bale. Ikiwa bado anahitaji kubaki United, basi inabidi amkumbushe kwamba yeye (Moyes) ndio boss na ikiwa atahitaji kupata nafasi basi atahitaji ni kujituma pekee ndio kutamfanya acheze mechi zote.

3 - KUJENGA TIMU YAKE MWENYEWE.
Ni muhimu kwa Moyes kujua kwamba hii timu sasa ni ya kwake, na japokuwa United walishinda ligi kwa urahisi kiasi na wachezaji ambao Fergie alikuwa akiwahusudu, lakini kwa Moyes inaweza ikawa tofauti. Pamoja Wascotland hawa kufanana kwa kiasi fulani - lakini ni watu wawili tofauti kabisa. Kwa kawaida lazima Mashabiki wa United watakuwa wameandamwa na kumbukumbu za Manchester United kwenye zama za Fergie, hili ni jambo la kawaida. Moyes haihtaji hii hali, kwa mara ya kwanza kwenye masiaha yake ya ukocha atakuwa na fedha nyingi za usajili. Ikiwa atazitumia vizuri na kwa umakini kwenye maeneo sahihi basi ataweza kutengeneza utawala mpya wa Manchester United katika zama zake na kutowapa watu sababu za kuangalia nyuma kwenye kwenye 'siku za ushindi'.

No comments:

Post a Comment