Search This Blog

Friday, May 31, 2013

HIVI NDIVYO MANCHESTER UNITED WANAVYOTENGENEZA MAMILIONI KWA SIKU KUPITIA WATALII WANAOKWENDA OLD TRAFFORD


Uwanja wa klabu ya Manchester United Old Trafford ndio kivutio cha kimichezo cha utalii maarufu kuliko vyote nchini Uingereza.

Karibia watalii millioni moja kutoka duniani kote walitembelea na kuangalia mechi kadhaa nchini Uingereza mwaka uliopita.

   
Johnstone Malunda

Kwa mujibu wa kitengo cha utalii hapa UK, watalii zaidi ya 900,000 kutoka nje ya UK walitumia kiasi cha £706 million, kwa wastani wa £785 kwa kila shabiki.

Old Trafford ndio iliongoza kwa kutembelewa ikifuatiwa na dimba la Liverpool - Anfield.
Uwanja wa Manchester City Etihad Stadium ulishika nafasi ya saba.

NAMNA OLD TRAFFORD INAVYOIINGIZIA MAMILIONI MANCHESTER UNITED 

Gharama za kufanya ziara ya saa moja ndani ya Old Trafford kwa kichwa ni paundi 16. Na kwa mujibu wa tour guide wa Old Trafford - watalii wapatao 1500 hutembelea uwanja wao kwa siku moja.

Kimahesabu uwanja huo unaitengenezea United paundi 24,000 kwa siku, ambazo ni sawa na paundi 168,000 kwa wiki na paundi millioni 8.6 kwa mwaka ambazo kwa pesa za madafu za kitanzania ni zaidi ya billioni 23. Hii ni pesa inayopatikana kupitia utalii tu wa Old Trafford.


Sota


Shabiki wa Man United Ismail Sota nilikuwa nae kwenye tour ndani ya Old Trafford.




No comments:

Post a Comment