Search This Blog

Wednesday, May 15, 2013

EUROPA LEAGUE FINAL: CHELSEA VS BENFICA - THE BLUES KUWEKA REKODI YA KUBEBA CHAMPIONS LEAGUE NA EUROPA LEAGUE MFULULIZO

Haijawa kutokea timu kuchukua ubingwa wa UEFA Champions League kisha kuchukua Europa League mfululizo, lakini hii ni rekodi ambayo Chelsea anaweza wakaiweka leo hii watakapocheza fainali ya Europa League na Benfica jijini Amsterdam Uholanzi. Katika kuelekea kwenye fainali hiyo tuangalie mambo muhimu kuhusu timu hizi mbili.

SAFARI YA TIMU ZOTE MPAKA KUFIKA FAINALI

Benfica
Ilishinda 1-0 vs Bayer Leverkusen
Ilishinda 2-1 vs Bayern Leverkusen
Ilishinda 1-0 vs  Bordeaux
Ilishinda 3-2 vs Bordeaux
Ilishinda 3-1 vs  Newcastle
Sare 1-1 vs Newcastle
Lost 1-0 vs Fenerbahce
Won 3-1 vs Fenerbahce

Chelsea
Ilishinda 1-0 vs Sparta Prague
Sare 1-1 @Stamford Bridge vs Sparta Prague
Walifungwa 1-0 vs Steaua Bucharest
Wakashinda 3-1 @Stamford Bridge Steaua Bucharest
Walishinda 3-1 Rubin Kazan
Wakafungwa 3-2 @Stamford Bridge vs Rubin Kazan
Walishinda 2-1 vs Basel
Wakashinda 3-1 @Stamford Bridge vs Basel
  
 

TAARIFA ZA TIMU

Benfica manager Jorge Jesus ana majeruhi mpya kwenye timu kuelekea fainali ya leo, ingawa mlinzi wa kulia Maxi Pereira amesimamishwa kwa kuwa na kadi za njano nyingi na hatocheza mchezo wa leo.
Chelsea boss Rafael Benitez tayari ameshathibitisha Eden Hazard hatocheza mechi ya leo na pia kuna wasiwasi kuhusu hatma ya John Terry.


BENFICA ITASHINDA IKIWA

Benfica wamefunga mabao 14 kwenye hatua za mtoano za Europa League, mabao sita yamefungwa na Oscar Cardozo.
Mparaguay huyo atakuwa miwba mchungu ikiwa atakuwa anapokea mipira mizuri kutoka kwa viungo wake, ingawa pia kuna hatari nyingine kwa Chelsea kutoka kwa Gaitan, Lima na Eduardo Salvio.
Katika safu ya ulinzi Benfica itabidi wacheze vizuri zaidi kuliko ilivyokuwa kwa Basel katika kuweza kuzuzia mashambulizi ya Chelsea - yenye watu hatari wanaoelewana kama Oscar, Juan Mata na Moses atakayechukua nafasi ya Hazard.

Fernando Torres anaweza kawa ndio mfungaji bora wa Chelsea kwenye michuano hii, lakini tishio la  Moses, Oscar na Juan Mata ambao watacheza nyuma yake ndio wakaisumbua sana safu ya ulinzi ya Benfica - na ikiwa Benfica wataweza kucheza vizuri dhidi watatu hao basi watakuwa wamejirahisishia kazi kwenye mchezo huo.

 CHELSEA ITASHINDA IKIWA
Inaonekana kama Chelsea wameweza kufika mpaka fainali lakini jasho haliwakuvuja la kutosha.
Ndio, kuna wakati walipata shida (hasa dhidi ya Rubin Kazan), lakini bado hawakuonekana kujali sana kuhusu kombe hili. na njia pekee ya kuweza kuwashinda Benfica walio kwenye bora kabisa itabidi wavuje jasho kweli kweli na kuweka umakini wao vizuri kwenye mechi ya leo.

Hazard, hatocheza leo, hivyo Mosses ambaye hutumia nguvu zaidi atachukua nafasi yake. Huku David Luiz akitarajiwa kucheza kwenye kiungo, hivyo The Blues watakuwa wapo vizuri kwenye ulinzi kiasi.

Wakati viungo wa Chelsea wanaokuwa kwenye kiwango chao, ni vigumu sana kushindana nao, ingawa mara nyingi inakuwa tatizo wanapocheza mabeki wa ulinzi imara na wenye kuelewana kama Luisao na Ezequiel Garay.
Gary Cahill na Branislav Ivanovic pia watakuwa na kazi ya kuhakikisha kijana wa kiparaguay na hatari Oscar Cardozo hakutani uso kwa uso na Peter Cech na kuwadhuru - Cordozo na hatari kwenye mipira hivyo itabidi wasimame nae kama wamegandanishwa nae na gundi.

 VIKOSI VINAVYOTARAJIWA

Benfica XI: Artur; Almeida, Garay, Luisao, Melgarejo; Matic, Perez; Salvio, Lima, Gaitan; Cardozo

 Chelsea XI: Cech; Azpilicueta, Ivanovic, Cahill, Cole; Ramires, David Luiz; Oscar, Mata, Moses; Torres

No comments:

Post a Comment