Search This Blog

Friday, April 19, 2013

BAADA YA MASHABIKI WAKE KUFANYA VURUGU UWANJANI - TIMU AEK ATHENS YASHUSHWA DARAJA

Moja ya klabu kongwe na kubwa nchini  Ugiriki AEK Athens imeshushwa rasmi daraja katika ligi kuu ya Ugiriki baada ya kukatwa pointi 3 kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wa klabu wikiendi iliyopita. 
 
Bodi ya nidhamu ya shirikisho la soka la Ugiriki lilikaa mapema leo na kutoa maamuzi hayo na pia timu pizani iliyokuwa inacheza nayo Panthrakikos imepewa ushindi wa 3-0.

Mashabiki wa AEK waliingia uwanjani baaada ya timu yao kuwa nyuma kwa 1-0 na mchezo ukasimamishwa kwenye dakika ya 88.

Huku wakiwa wamebakiwa na mchezo mmoja, adhabu ya kukatwa pointi 3 inamaanisha AEK itamaliza wapili kutoka chini hivyo kushuka daraja.

Timu hiyo pia imekatwa pointi 2 kwa msimu ujao na kupigwa faini ya $9,100.

No comments:

Post a Comment