Search This Blog

Thursday, March 14, 2013

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAZINDUA KAMPENI MPYA YA TUPO PAMOJA.



Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo akiongea na waandishi wa
habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bia ya Serengeti ya "Tupo pamoja
katika shangwe za mafanikio" hii leo
Ratiba

Machi 14, 2013, JB BELMONTE, DAR ES SALAAM:   Leo katika hafla iliyohudhuriwana waandishi wa habari, wageni na wadau mbalimbali Kampuni ya bia ya Serengeti imezindua kampeni mpya na ya kipekee inayoenda kwa kauli mbiu ya TUPO PAMOJA.  Katika hafla hiyo iliyofana asubuhi ya leo pia ilihudhuriwa na wadau wa bia hii katika ishara ya kushereheka mafanikio na shangwe za bia hii.

Akiongea na waandishi wa habari asubuhi la yeo, Mkurugenzi wa mMasoko wa kampuni ya bia Serengeti Bw. Ephraim Maguru alisema kwamba, “ kwa miaka kumi saa, tumeona na kushuhudia ukuaji na mafanikio makubwa”.  Bia hii inajulikana kwa kampeni ya ‘raha kamili kwa wengi wanaifahanu kama Chui.  Pia kwa udhamini wa Taifa stars ambao uliinua hadhi ya soka la Tanzania kwa kiwango kikubwa.  Kuna ufadhili wa Fiesta, ambao wote mnajua mchango Fiesta inatoa katika ukuaji wa tasnia ya muziki wa kizazi kipya hapa nchini.  Aliendelea Bw. Mafuru

 Bia ya Serengeti ni bia ya kipekee ambayo ndio bia ya kwanza Tanzania yenye kimea halisi kwa asilimia mia.    Mwaka jana bia hii pia ilizindua muonekano mpya  wa nembo yake huku ikibaki na ladha ile ile.  Baada ya utafiti, Kampuni ya bia ya Serengeti na wadau wake, wamebaini kwamba watanzania wanahitaji  shangwe za mafanikio yao katika sekta mbalimbali zikiwemo za uchumi, kijamii, kimichezo na kadhalika.

“Tunawakaribisha wote katika hafla mbali mbali ambazo tutaandaa ili kueneza kampeni hii ya Tupo Pamoja kama mlivyoona katika matangazo niliyowaonyesha, tutaleta shangwe popote mlipo., Alieleza meneja wa kinywaji hicho Bw. Allan Chonjo,  baada ya kuonyesha matangazo mbali mbali yatakovyokuwa katika vyombo vya habari.

Hafla hiyo ya uzinduzi pia ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa Kampuni ya bia ya Serengeti wakiwemo wasambazaji wa bia.  Kampeni hii inawatambua na kuwathamini  watanzania wote  kwa mafanikio yao katika sekta mbalimbali za maendeleo.


Kampuni ya bia ya bia ya Serengeti inajihusisha na biashara ya  vinjwaji vyenye vileo  kama bia- Premium Serengeti Lager, Tusker Lager, Tusker Malt Lager, Tusker Lite, Uhuru Peak Lager, Pilsiner,  Guinness na vinywaji vikali kama  Johnnie Walker, Smirnoff Vodka, Richot, Bond 7 and Gilbeys. Pia vinywaji visivokuwa na kileo kama Malta Guinness
Serengeti Breweries Limited is subsidiary of EABL/ DIAGEO.


Kwa maelezo zaidi wasiliana na Mkurugenzi wa Mawasilianao na Mahusiano  SBL: Email: evans.mlelwa@serengetibrew.com Meneja Mawasiliano- SBL   imani.lwinga@serengetibrew.com

No comments:

Post a Comment