Search This Blog

Saturday, February 23, 2013

UHAMISHO WA STOPPILA SUNZU READING WAKWAMA - SUNDERLAND WAMTAMANI

Itabidi Sunderland wavunje benki ili kuweza kushinda vita ya kugombea saini ya Stoppila Sunzu kutoka klabu ya Congo TP Mazembe. 

Sunderland wamekuwa wakihusishwa na suala la kumsajili beki huyo wa kati, ingawa mdogo huyo wa mshambuliaji wa Simba Felix Sunzu ameshafanya mazoezi na Reading mwezi uliopita.


Lakini uhamisho wa mchezaji huyo kujiunga na Reading ukaingia na mtafaruku kutokana na mkanganyiko wa mkataba wake, wakati wawakilishi wa mchezaji na mchezaji mwenyewe wakisema hawana mkataba na TP Mazembe lakini kumbe ilikuwa tofauti.

Mmiliki wa TP Mazembe Moise Katumbi: "Suala la mkataba wa Sunzu lilishawekwa sawa baada ya kuupitia vizuri mkataba na mchezaji na wawakilishi wake wakakubali kwamba mkataba bado ulikuwa hai baina yetu. 


"Tatizo ni kwamba wawakilishi wake wamekuwa wakimdanganya ili aende kinyume dhidi yetu. Tunahisi wanataka kuchukua ada yote ya uhamisho kwa kusema kwamba ni mchezaji huru. 

"TP Mazembe ni professional club na hatutojaribu kuzuia haki za mchezaji yoyote ili mradi tu afuate sheria na kanuni zote. 

"Kama kuna klabu inamtaka mchezaji huyu, wawasiliane na sisi na hakika hatutomzuia kuondoka lakini hizo au hizo klabu inabidi ziongee kwanza na sisi kama sheria isemavyo."

No comments:

Post a Comment