Search This Blog

Friday, February 8, 2013

TUTAIFUNGA TOTO AFRICANS KESHO- SELEMBE

Kweli siyo nzuri kwetu lakini sio  mbaya tumeanza vizuri lakini sisi malengo yetu ni nafasi za juu kwa hiyo mapambano yanaendelea mpaka mwisho” anasema kiungo wa pembeni wa timu ya soka ya Coastal Union iliyopo katika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara. Coastal ambayo itasafiri na kwenda kuwakabili Toto Africans ya Mwanza hapo kesho katikas uwanja wa CCM Kirumba .
‘ Tuliwafunga Toto kaatika mchezo wa kwanza,  na nategeme kuwafunga tena unajuwa , Mwanza mbali lakini tuta safiri kwa ndege HILO  ni jambo zuri kwetu tuta punguza uchovu’ anasema, Selembe na kuongeza
Nikweli kutakuwa na ugumu katika mchezo kwa sababu ni ngumu sana kushinda katika uwanja ule ( Kirumba) lakini Coastal imejipanga vizuri msimu huu na dhamira yetu ni kuwa miongonui mwa timu mbili za juu, hali ya wachezaji wenzangu pamoja na ile ya viongozi ndiyo inayo nifanya nijiamini kuwa titashinda”
“Wamuzi mpaka sasa kwa upande wetu wamejitahidi ila makosa ya kibinadamu yapo huwezi kuwalaumu sana lakini mpaka sasa wanakwenda vizuri wajitahidi kwani wao ndiyo muhimili wa soka letu” anamaliza kiungo huyo wa timu ya taifa ya Zanzibar

No comments:

Post a Comment