Search This Blog

Tuesday, February 12, 2013

STEPHENI KESHI ABADILI UAMUZI - KUENDELEA KUWA KOCHA WA NIGERIA


Shirikisho la soka la Nigeria limesema leo Jumanne kwamba Kocha wa timu ya taifa Stephen Keshi amebadili uamuzi wake wa kujiuzulu na mazungumzo baina yao na kocha huyo yanaendelea baada ya kocha huyo kuiwezesha Nigeria kushinda ubingwa wa Afrika.

Keshi na Super Eagles, ambayo waliifunga Burkina Faso 1-0 Sunday  na kushinda AFCON 2013, wanatarajiwa kuwasili Nigeria leo huku wakiwa wameandalia sherehe na raisi wa nchi huko mjini Abuja.
    Kujiuzulu kwa Keshi, amabye alitangaza uamuzi wake jana kupitia radio moja huko South Africa, kumeleta aibu kwa utawala wa soka wa nchi hiyo, ambayo imekuwa kiandamwa na skendo za rushwa na utawala mbovu kwa miaka kadhaa sasa.

Shirikisho hilo lilitoa taarifa leo asubuhi kuhusu kujiuzulu kwa Keshi, na kusema kwamba kocha huyo amebadilisha uamuzi wake.

Keshi alisema jana kwamba ameamua kujiuzulu kwake kumekuja kutokana na maofisa wa NFA kumtishia kumfukuza kazi kabla ya mechi ya robo fainali dhidi ya Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment