Search This Blog

Thursday, February 7, 2013

SIMBA YAMRUHUSU OBADIA MANGUSA KUKIPIGA AFRICAN LYON


Baada ya kusota kwa muda mrefu hatimaye mlinzi, Obadia Mungusa atakuwa huru kuitumikia timu ya African Lyon hadi mwishoni mwa msimu huu.

 Simba iliiandikia barua timu ya Lyon siku ya jana na kutoa ruhusa kuwa sasa wanaweza kumtumia mlinzi huyo aliyekosa nafasi klabuni, Simba walau hadi mwisho wa msimu huu. " Jana nilipigiwa simu na uongozi wa Lyon kuwa Simba imeniruhusu kuichezea timu yao hadi mwishoni mwa msimu kwa mkopo" anathibitisha, Mungusa wakati akiongea na tovuti hii asubuhi ya leo. Obadia ambaye alitibuana na makamu mwenyekiti wa timu hiyo, Geofrey Nyange Kaburu kuelekea mwishoni mwa mzunguko wa kwanza kwa sababu za kimaslai na kuamua kujiondoa klabuni hapo baada ya kupeleka madai ya mshahara wake na pesa za usajili ambazo aliahidiwa kupewa wakati akijiunga na mabingwa hao watetezi wa ligi kuu akitokea Mtibwa Sugar miaka miwili iliyopita. 

Ameondoka Simba huku akidai mshahara wa miezi mitano.  "Nimeondoka ili kunusuru kipaji changu, japo bado nawadai mshahara wa miezi mitano" anasema

No comments:

Post a Comment