Search This Blog

Thursday, February 7, 2013

EDWARD CHRISTOPHER: NAREJEA DIMBANI HIVI KARIBUNI KUISADIA SIMBA KUTETEA UBINGWA


Mshambuliaji chipukizi wa timu ya taifa na klabu ya soka ya Simba ambaye ni majeruhi kwa takribani, mwezi mmoja sasa, Edward Christopher, amesema anaendelea vizuri japo bado anasikia maumivu kwa mbali. 

Edo ambaye aliumia akiwa katika michuano ya Mapinduzi huko Visiwani Zanzibar mwanzoni mwa mwezi uliopita, alisema hayo mapema siku ya leo wakati akizungumza na tovuti hii. 
"Ninaendelea vizuri, lakini bado ninasihisi maumivu katika mguu wangu" anasema mshambuliaji huyo anayesubiliwa kwa hamu na mashabiki wa klabu yake ambayo inahaha kutetea ubingwa wake wa ligi kuu ya Vodacom.

" Mashabiki wawe na uvumilivu kwani muda si mrefu nitarejea uwanjani" anaongeza kusema kinda huyo ambaye wengi wanataraji ataziba pengo la mshambuliaji, Mganda, Emmanuel Okwi ambaye ameuzwa katika klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia, mwezi uliopita. Edo alitwaa tuzo ya ufungaji bora wa michuano ya Super8, agosti mwaka jana.

No comments:

Post a Comment