Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

HATIMAYE TAIFA STARS WAKABIDHIWA BASI LAO LA MIL.200 NA KILIMANJARO

HATIMAYE  Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro imeikabidhi Timu ya Taifa(Taifa Stars)basi jipya la kisasa lenye thamani ya Sh 200 litakalotumika kwa safari za timu hiyo.

Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika makao makuu wa TBL jijini Dar es Salaam jana na kuhudhuriwa na maofisa wa ngazi za juu wa TFFna baadhi ya wadau wa soka.


TBL ilikabidhi basi hilo kama sehemu ya utekelezaji wa udhamini wake kwa timu hiyo ulioingiwa Mei mwaka jana kati yake ya Shirikisho la Soka Tanzani(TFF).

Akizungumza wakati wa hafla hiyo,Meneja  wa Bia Kilimanjaro,George Kavishe alisema kuwa basi hilo kutoka kampuni ya Yutong limezingatia vigezo kwa matumizi ya timu ya taifa.

"Wachezaji wetu lazima wawe na nafasi nzuri ya kupumzika wakati wa safari ,na hiyo ndiyo sababu iliyotufanya tununue basi hili la kisasa,tunaomba mlitunze,".alisema Kavishe.

Kwa upande wake Rais wa TFF,Leodegar Tenga aliishukuru TBL kwa kukabidhi basi hilo na kusema shirikisho lake litaendeleza kutekeleza yale yote yaliyomo katika mkataba baina ya pande hizo mbili.

"Ahadi yangu ni kwamba  TFF itaendelea kushirikiano nanyi sambamba na kutekeleza yake yote yaliyomo katika mkataba baina yetu,".alisema Tenga.

No comments:

Post a Comment