Search This Blog

Friday, February 1, 2013

EMMANUEL OKWI AANZA KWA KUWAFUNIKA MASTAA WENZAKE WALIOSAJILIWA NA ETOILE DU SAHEL


EMMANUEL Okwi ameanza vizuri katika kikosi chake kipya cha Etoile du Saleh ya Tunisia, baada ya kuwafunika mastaa wenzake watatu waliosajiliwa katika majira ya baridi.


Mtandao wa klabu hiyo Etoile-du-Sahel.com umewashindanisha Okwi raia wa Uganda aliyesajiliwa kutoka Simba pamoja na 

Mtunisia Oussema Boughanmi, Akoli Percy mshambuliaji wa Congo na Manzie Bidge kuwa nani mkali.
Ambapo mashabiki 367 walioanza kupiga kura kuanzia Januari 18 hadi leo Ijumaa wamemchagua Okwi kwa kura 225.


Mtunisia Oussema ambaye ni kiungo mkabaji yeye anafuatia baada ya kupigiwa kura 99, wakati Manzie amepata 27.


Akoli kutoka Congo ndiye anayeshika mkia baada ya kupigiwa kura za ndiyo 16 tu kwa mashabiki wote.


Kupata kura hizo ni kutokana na jinsi anavyowavutia mashabiki hao katika uwajibikaji wake kwenye mazoezi na mechi.

No comments:

Post a Comment