Search This Blog

Friday, December 28, 2012

JINA LA ZLATAN LAONGEZWA KATIKA KAMUSI YA SWEDEN

 

2012 - umeendelea kuwa mwaka mzuri kwa Zlatan Ibrahimovic, baada ya kupata mafanikio ya uwanjani na kiuchumi sasa jina lake limeongezwa katika kamusi ya kisweden na taasisi inayoshughulikia lugha nchini Sweden - Neno 'Zlatanera' lenye maana ya Zlatan au 'kutawala' limeongezwa katika kamusi rasmi ya Sweden.

Hii imekuja kama kumtunuku mchezaji huyo ambaye amekuwa akiletea sifa nchi hiyo ndani na nje ya nchi hiyo kwa miaka takribani 10 sasa.

Neno 'Zlatanera' limetokana na neno la kifaransa 'zlataner' lenye maana ya kutawala, hivyo wasweden wakalinyambua na kuongeza herufi 'a' katika 'zlataner'.

No comments:

Post a Comment