Search This Blog

Friday, November 9, 2012

SERGIO RAMOS: BILA MAMA NINGEKUWA NACHEZA MCHEZO WA KUPIGANA NA NG'OMBE NA SIO SOKA

 
Sergio Ramos amevunja ukimya juu ya ushangiliaji wake wa alioufanya wakati akishangilia ubingwa wa ulaya wa Spain mwaka huu.
Mlinzi huyo wa Real Madrid hajawahi kuficha hisia zake alizonanzo juu ya mchezo wa kupigana na ng'ombe ambao ni maarufu huko kwao Spain. Baada ya mafanikio yake ya uwanjani Sergio huonekana akicheza dansi za aina fulani huku akiwa na kitambaa kikubwa, lakini sasa anasema kwamba chaguo lake lilikuwa kucheza mchezo huo badala ya soka kama mama yake asingeingilia kati.
"Unapokuwa mdogo ni muhimu kuwa na ndoto," anaiambia AS.
"Ndoto yangu kubwa siku zote ilikuwa ni kuwa mcheza mchezo wa kupigana na ng'ombe au mwanasoka, lakini mama yangu hakupenda mie nicheze mchezo huo kwa sababu ni hatari, hivyo nikaona bora nicheze soka kwa sababu haukuwa mchezo wa hatari kama wa kupigana na ng'ombe."

No comments:

Post a Comment