Search This Blog

Thursday, November 29, 2012

NDOTO ZA UBINGWA WA 6 WA DUNIA - BRAZIL YAWARUDISHA SCOLARI NA CARLOS ALBERTO KILINGENI

Luiz Felipe Scolari ametangazwa kuwa kocha mpya wa wenyeji wa Kombe la Dunia 2014 Brazil leo, akirejea katika benchi la ufundi la nchi yake kwa mara ya pili katika jaribio la kutwaa ubingwa wao wa sita kwenye ardhi ya nyumbani ndani ya kipindi cha miezi 18 ijayo.

Scolari, ambaye aliiongoza Brazil kutwaa taji lao la tano na la mwisho la dunia katika fainali za mwaka 2002 - miaka 10 iliyopita, alitambulishwa rasmi na Shirikisho la Soka la Brazil kwenye mkutano na waandishi wa habari, akichukua nafasi iliyoachwa na Mano Menezes aliyetimuliwa Ijumaa iliyopita.

Carlos Alberto Parreira, ambaye aliiongoza Brazil kutwaa ubingwa wao wa nne wa dunia mwaka 1994, alitangazwa kuwa mkurugenzi wa ufundi wakati shirikisho hilo la soka la BraziL.

No comments:

Post a Comment