Search This Blog

Saturday, November 10, 2012

EPIQ BSS YAMALIZIKA NA USHINDI WA WALTER CHILAMBO

Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akikabidhiwa sanduku lake lenye kitita cha shilingi milioni 50 ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee,katika shindano hilo lililovuta hisia za wengi,mshindi wa pili ameibuka mwanadada Salma Abushiri  (Zanzibar) na watu ni Wababa Mtuka (Dar).

Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akiwashukuru wapenzi na msahabiki wake waliompigia kura na hatimaye kuibuka mshindi wa shindano hilo,lililofanyika ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee.

Baadhi ya mashabiki wa mshindi wa shindano hilo la EBSS,Walter Chilambo wakishangilia kwa shangwe na vifijo mara baada kutamkwa yeye ndiye kinara katika kilele cha shindano hilo lililovuta hisia za watu wengi.

Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, na Jaji Mkuu wa Shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), akiwa amemkumbatia mshindi wa shindano hilo Walter Chilambo ndani ya ukumbi wa Diamond,Chilambo ameibuka na kitita cha shilingi Milioni 50.

Msanii Barnaba akiimba na mmoja wa washiriki wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS).

Mshiriki wa EBSS NshomaNg'hangasamala akiimba moja ya wimbo wake jukwaani.

Mwanadada Salma Albushiri akiimba kwa hisia huku akipiga gitaa mbele ya mashabiki wake waliofika kumshuhudia ndani ya ukumbi wa Diamond.

Mapouda.! majaji hawaishi vituko. Picha kwa Hisani ya Father Kidevu Blog

No comments:

Post a Comment