Search This Blog

Wednesday, November 21, 2012

DROGBA AOMBA KUSAJILIWA KWA MKOPO - KURUDI CHELSEA??

DIDIER DROGBA amefungua mlango wa kurudi kwenye premier league baada ya kuomba ruhusa ya kujiunga na klabu nyingine nje ya dirisha la usajili.

FIFA ilisema kwamba inafikiria ombi la mshambualiaji wa Shanghai Shenhua katika siku moja ambayo kocha wa zamani wa Chelsea Di Matteo alipofukuzwa.
  Taarifa ya FIFA ilisema: “Tunaweza kuthibitisha kwamba mchezaji Didier Drogba ametuma ombi la kuruhusiwa kusajiliwa nje ya dirisha la usajili na klabu kwa mkopo."


Drogba, ambaye aliondoka Chelsea baada ya kufunga penati ya ushindi katika fainali ya champions league, amekuwa akifikiria kurudi kufanya mazoezi na klabu yake ya zamani wakati ligi kuu ya China itakapokuwa imeisha - kitu ambacho Di Matteo alisema atakukaribisha vizuri kabla ya kutimuliwa leo asubuhi.
Kwa sheria zilizopo za FIFA haziruhusu Drogba kuhamia timu yoyote mpaka January 1.

No comments:

Post a Comment