Search This Blog

Thursday, November 22, 2012

BINAMU YAKE MESSI AMPELEKA FIFA RAISI WA KLABU YAKE KWA KUMTOLEA MANENO YA UBAGUZI WA RANGI

Wakati Lionel Messi akiendelea kuweka rekodi za kufunga - akiongeza mawili na kumpita Ruud Van Nisterlooy kama mfungaji bora wa pili katika historia ya Champions league  - binamu yake, Maxi Biancucchi, amemtuhumu Raisi wa klabu ya Paraguay kwa ubaguzi wa rangi.

Raisi wa Olimpia Marcelo Recanate anatuhumiwa kwa kumtukana Biancucchi baada ya mchezaji kusema anafikiria kuhamia nchini Qatar. 

“Tumetuma barua na nyaraka zote. FIFA watazipokea leo," wakili wa Biancucchi aitwaye Ricardo Scarane aliiambia Radio 970 AM.
“Maxi anayajua yote yaliyosemwa. Ameumizwa sana na maneno ya Marcelo lakini ataendelea kutimiza matwaka ya mkataba wake kwa mapenzi aliyonayo kwa timu na mashabiki wa klabu."

No comments:

Post a Comment