Search This Blog

Friday, November 23, 2012

BAADA YA DI MATTEO - MARK HUGHES NAE AENDA MAJI QPR

MARK HUGHES ametimuliwa kazi ya kuwa kocha wa QPR.

Mmiliki wa QPR Tony Fernandes amemfukuza kazi kuelekea mchezo dhidi ya Manchester United.
Harry Redknapp ndiye mtu ambaye anatajwa kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Hughes pale Loftus Road.
  Taarifa rasmi ya QPR statement ilisema: "Uamuzi huu umechukuliwa kwa uangalifu mkubwa na bodi ya wakurugenzi, kufuatia mikutano iliyofanyika kwa siku kadhaa zilizopita.

"Bodi ya wakurugenzi inamtakia kila la kheri na kumshukuru Mark kwa aliyoifanya katika kipindi cha miezi 10 iliyopita.
"Mark ameonyesha ueledi na uaminifu katika kipindi chote alichokuwa hapa, lakini kwa hali iliyopo tumejikuta hatuna chaguo zaidi ya kufanya mabadiliko.
"Bodi sasa itafanya kazi kwa nguvu katika kuweka meneja mpya kwa haraka zaidi."

No comments:

Post a Comment