Search This Blog

Friday, October 19, 2012

UCHAMBUZI LIGI KUU RAUNDI YA 8: YANGA, KAGERA SUGAR COASTAL UNION, NA MTIBWA SUGAR AKA FC PORTO YA TANZANIA



YANGA SC
Msimu uliopita ilikumbwa na kirusi kikubwa cha migogoro ya kiuongozi ambayo ilichangia matokeo mabovu katika ligi na kuangukia nafasi ya tatu mwishoni mwa msimamo.


 Imejiimarisha kwa kuongeza wachezaji muhimu kwenye nafasi ambazo zilikuwa na mapungufu. Walishtuliwa mapema kwenye ligi baada ya suluhu-pacha siku ya ufunguzi wa msimu dhidi ya Tanzania Prisons na kukutana na kipigo kizito cha mabao 3-0 mbele ya Mtibwa Sugar.

 Wameimarisha na kupandisha kiasi kiwango chao cha uchezaji, huku urejeo wa majeruhi kama, Nurdin Bakary ukirejesha wingi wa machaguo bora kikosini. Imeweza kupanda haraka juu ya msimamo hadi nafasi ya tatu, pointi nane nyuma ya vinara na mahasimu wao Simba ambao wapo kileleni, lakini Yanga wana nafasi ya kufuta ‘gepu’ hilo wakati watakapocheza mchezo wao wa nane dhidi ya Ruvu Shooting hapo jumamosi, kama wakishinda watakuwa nyuma ya vinara kwa tofauti ya pointi tano tu.

UDHAIFU WAO
Yanga inafundishwa na kocha wa nne kwa kipindi cha miezi 12 tu. Alianza, Sam Timbe, akafuatia, Kostadin Papic, kisha Tom Saintfiet na sasa Ernest Brandts. Ni tatizo na udhaifu mkubwa wa timu hii kwa miaka ya karibuni, ingawa wamekuwa wakisajili kwa kiasi kikubwa cha pesa kwa miaka mitano iliyopita, Yanga imeshindwa kuwa timu imara kutokana na mabadiliko yasiyostahili ya makocha, wakati na muda wa kuingia na kutoka kwa makocha ndani ya timu hii huwa si mwafaka. 


UTABIRI. Wanaweza kurejea juu ya msimamo kama watani wao Simba hawatachanga vyema karata zao pale watakapokuwa ugenini dhidi ya Prisons, JKT Mgambo na Polisi Moro. Mategemeo watakuwepo kwenye Top 3.


MTIBWA SUGAR. FC PORTO YA TANZANIA INAYOOGOPA KIVULI CHAKE.
Wakati wanatwaa mataji mfululizo ya ligi kuu katika miaka ya 1999 na 2000, Mtibwa ilitambulisha vipaji kadhaa ambavyo vilitamba katika soka la Tanzania kwa miaka kadhaa, Mecky Mexime, Kassim Issa, Geofrey Magori, Abuubakary Mkangwa na wengine wengi ambao baadae walijiunga na vilabu maarufu vya Yanga na Simba, hata nyakati za kina Nico Nyagawa. Mussa Mgosi na sasa kina Hussen Javu, Babuu Ally na chipukizi kadhaa waliopo katika kikosi cha sasa ni mfano tosha kuwa timu hii kwa kipindi cha miaka 12 isiyo na taji la ligi kuu, imeweza kunufaika na uuzaji wa wachezaji. Wakati bingwa wa ligi kuu akitarajiwa kuingiza zaidi ,illion 70, Mtibwa inaingiza pesa hizo kwa kuuza wachezaji tu.

Mara kadhaa msemaji wa timu hiyo, Thobias Kifaru amekuwa akisisitiza hadi pale haki itakaporejea katika soka la Tanzania ndiyo wataweza kutwaa tena taji la ligi kuu, lakini kwa sasa si rahisi kufanikiwa katika hilo kutokana na aina ya ushindani uliopo katika ligi yetu, Kifaru amekuwa akisisitiza kuwa timu yao ni bora hata zaidi ya Simba na Yanga. Mwenendo wao bado si wa kuridhisha sana katika ligi, na mara baada ya kufungwa na Mgambo wikiendi iliyopita katika uwanja wao wa nyumbani, watakuwa Mkwakwani, Tanga kucheza na Coastal Union, jumamosi hii.


UDHAIFU WAO.
Wanawahi kukata tamaa mapema na imepoteza uwezo wake wa kushinda katika uwanja wao wa Manungu Complex.

COASTAL UNION.
Wana utajiri na wapo katika umbo zuri la ushindani hadi sasa. Mara ya mwisho klabu hii kutwaa taji ni mwaka 1988, pale walipotwaa taji la ligi daraja la kwanza ( sasa ligi kuu). Wamejiimarisha vizuri kiuchumi na kimaandalizi na wakati tayari wamecheza michezo saba, Coastal wamepoteza mara moja na kushinda michezo miwili, huku sare ikiwa imetoka mara nne. Wachezaji wa timu hiyo ni wale ambao walipata kuzichezea klabu za Simba, Yanga na Azam kwa vipindi tofauti. Tayari wamefanya mabadiliko katika benchi lao la ufundi kwa kumtoa, Juma Mgunda na kupewa kazi, Hemed Morocco. Ina wachezaji kama nahodha, Said Sued, Juma Jabu, Jerry Santo, Pius Kisambale, Nsa Job, Atupe Aggreen.
Ukizungumza na wachezaji wa timu hiyo wanadai wanataka kuwemo ndani ya nafasi mbili za juu, kitu ambacho kinamaanisha, Yanga, Simba, Azam au Mtibwa kugombea nafasi moja ya juu kati ya mbili. Ni ngumu na wakiwa tayari wameonesha kutokuwa imara katika uwanja wa nyumbani, Coastal inatakiwa kuonesha vitendo uwanjani na si maneno.
UTABIRI. Wana matarajio makubwa akilini mwao, lakini wanatakiwa kuangaza macho zaidi ili kuona kilichopo mbele yao, kama wataendelea kuangusha pointi nyumbani, watapata wakati mgumu wakienda, Morogoro kucheza na Mtibwa na Polisi, vipi kuhusu uwanja wa Kaitaba na sapoti wa wakazi wa Mwanza kwa Toto? Kisha watatakiwa kuja Dar es Salaam mara sita kwa msimu.


UTABIRI; Kama wasipokuwa makini watajikuta wakipigania kutoshuka daraja mwishoni mwa msimu, ni lazima wakusanye pointi za nyumbani ili kuwa salama.


KAGERA SUGAR;
Chini ya kocha Abdalah Kibadeni, Kagera inacheza soka safi lenye kuvutia, wachezaji wake hawakati tamaa, na wana hali kubwa ya ushindi, kuanzia kwa nahodha, Amandus Nesta, Maregesi Mwangwa, Salum Kanoni, Shija Mkina na utitiri wa vipaji chipukizi, timu hiyo iliweza kutoka nyuma ya mabao 2-0 dhidi ya Simba na kupata pointi moja muhimu katika uwanja wa Taifa. Wamejiimarisha vizuri kuanzia katika utawala hadi ndani ya uwanja. Kuwaondoa wachezaji kama Hussein Sued ilikuwa ni uamuzi mzuri ili kusajiliwa kwa Mnigeri, Enyina Darrington ambaye anaisaidia sana timu hiyo.


UTABIRI;  Timu kama hii unaweza kuifananisha na Everton kwa pale England, huwezi kujua watamalizia wapi mwishoni mwa msimu, imekuwa na udhaifu wa kushindwa kumaliza ligi vizuri na mara mbili walikosa ubingwa baada ya kushindwa kumaliza ligi. Wanawania nafasa ya kucheza michezo ya Super8 msimu ujao hivyo wanaweza kufanya lolote na kuwemo ndani ya ‘top 3’

No comments:

Post a Comment