Search This Blog

Wednesday, October 24, 2012

TEKNOLOJIA YA MSTARI WA GOLI KUANZA KUFUNGWA KWENYE VIWANJA VYA SOKA DUNIANI KOTE BAADA YA FIFA KUSAINI MKATABA RASMI

Teknolojia ya mstari wa goli kwenye viwanja vya soka imekaribia kuanza baada ya leo FIFA kusaini mkataba na makampuni mawili makubwa yatakayosimamiwa teknolojia hiyo.

GoalRef na Hawk-Eye wamepewa ruhusa ya kuanza kufunga mifumo yao ya teknolojia dunaini kote baada ya kusaini mkataba huo na chombo kinachosimamia soka ulimwenguni.

Taarifa ya FIFA ilisema: “Kuanzia October 2011 mpaka June 2012, kampuni zote mbili zilipita katika majaribio ya nje ya ya maabara, pia majaribio katika mechi za moja kwa moja.
"Mjaribio yote yalifaulu kwa maana hiyo sasa mchakato huu ulioanza mwaka 2011 unakaribia kumalizika, na kampuni zote mbili zimepewa mamlaka ya kufunga teknolojia hiyo dunini kote." 

Lakini FIFA wakasema pia kwamba: "Pindi teknolojia hiyo inapofungwa uwanjani, itafanyiwa uchunguzi kuangalia namna inavyofanya kazi.

"Uchunguzi huo utafanywa na taasisi huru na majibu yatakayotolewa lazima yawe chanya juu ya mashine hiyo na hapo ndipo pekee teknolojia hiyo inaweza kutumika katika mechi rasmi."

No comments:

Post a Comment