Search This Blog

Thursday, October 11, 2012

MIAKA 75 BAADA YA GWIJI LA MANCHESTER UNITED BOBBY CHARLTON KUZALIWA - MFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA MASHETANI WEKUNDU

Siku kama ya leo miaka 75 iliyopita alizaliwa kiungo mshambuliajimstaafu wa Manchester United na timu ya taifa ya England Sir Bobby Chalton.

Sir Bobby ambaye kwa sasa ni mwanachama wa bodi ya wakurugenzi wa Manchester United ni mmoja kati ya wachezaji wachache walioichezea United mechi nyingi na kufunga mabao mengi, anashika nafasi ya pili nyuma ya Ryan Giggs kwa kucheza mechi nyingi, akiitumikia United katika mechi 758 na kuweza kuifungia mabao 249, akiwa anaongoza katika listi ya wafungaji bora wa muda wote wa klabu ya Manchester United.





Bobby Charlton ni mmoja kati ya wachezaji wanne wa Red Devils ambao wameshawahi kushinda tuzo ya uchezaji bora wa dunia - wa kwanza alikuwa Dennis Law 1964,  akafuatia Charlton 1966, George Best mwaka 1968 na mwaka 2008 Cristiano Ronaldo.
Charlton akiwa na Fergie mwaka 2011

Charlton pia ndio mfungaji bora wa muda wote wa England akiwa ametupia mabao 49 katika mechi 106.

Charlton alikuwa mmoja wa wachezaji waliopata ajali ya ndege wakati United jijini Munich.

Pia siku kama ya leo mwaka mmoja uliopita Shaffih Dauda nilibahatika kupata mtoto wangu wa pili aitwaye Dauda Jr aka Solskjaer ambaye anashea siku moja ya kuzaliwa na mke wangu pia.


Happy Birthday Legend, Happy birthday Wife, Happy Birthday Dauda Jr Solskjaer.


  HII NDIO MAKALA YA VIDEO INAYOELEZEA MAISHA YAKE YA SOKA KIUJUMLA

No comments:

Post a Comment