Search This Blog

Thursday, October 11, 2012

FULL TIME: TOTO 1:3 YANGA



Leo kuna Mchezo mmoja wa ligi kuu ya VODACOM Tanzania Bara, mchezo huo unapigwa kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza kati ya Toto Africans na Yanga.
Blog yako inakupatia baadhi ya matukio live ya mchezo huo.

Dk 36: yanga inaongoza kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na mshambuliaji Didier Kavumbagu pamoja na beki Mbuyu Twite.

Dk : 40 Toto wanakosa bao baada ya shuti kali kupaa kidogo juu ya lango.

Dk : 42 Toto wanapata penalti

Dk : 43 Toto wanakosa penalti,Emanuel Swita amepiga nje kulia mwa golikipa Yew Berko

Dk : 45  zimeongezwa dk 2 za nyongeza.

MPIRA NI MAPUMZIKO

TOTO 0:2 YANGA.

Kipindi cha pili kimeanza.

Dk 46: yanga walipata kona iliyopigwa na Haruna Niyonzima lakini haikuzaa matunda.

Dk 50: Toto wanafanya mabadiliko anaingia Mohamed Chingo badala ya  Haruna Athumani

Dk 52: Toto wamepata kona wakaipoteza,\

Dk 54: gooooooooooooooooooooooooooooooooo! Toto Africans wanapata bao,Mussa Said ndiye aliyeifungia Toto bao baada ya mabeki wa Yanga kushindwa kuelewana.

Dk 61: Toto wamekosa bao la wazi,lilipigwa shuti na kiungo Emanuel Swita golikipa wa Yew Berko akapangua mshambuliaji Mussa akapiga nje goli likiwa wazi.

Dk 64 : Yanga wanafanya mabadiliko,viungo Athuman Idd na Frank Domayo wametoka na nafasi zao zimechuliwa na Shamte Ally na David Luhende.

Dk 68: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! Jerry Tegete anaipatia YANGA bao la 3, pasi nzuri toka Didier Kavumbagu jerry Tegete akauwahi mpira kwenye eneo la mita 18 akampiga kipa chenga na kupasia nyavu, Hili ni bao la kwanza la msimu la Tegete.

Dk 85: Emanuel Swita wa Toto anapewa kadi ya njano, Swita pia aliwahi kuichezea Yanga kwa msimu mmoja kabla ya kurejea Toto Africans.

FT: TOTO 1:3 YANGA

1 comment:

  1. Jerry kafufukia kwa baba ake duh kama sinema vile hatuna njinsi hongereni watan

    ReplyDelete