Search This Blog

Wednesday, October 10, 2012

MCHEZAJI WA AC MILAN AWA WAZIRI MKUU MSAIDIZI NA WAZIRI WA MIUNDOMBINU NCHINI GEORGIA



Mchezaji wa zamani wa AC Milan Kakha Kaladze amethibitishwa kuwa waziri mkuu msaidizi wa nchi ya Georgia.

Mshindi wa mara mbili wa UEFA Champions league  akiwa na Milan, Kaladze amekuwa makamu wa waziri mkuu na pia waziri wa miundo mbinu na maendeleo katika serikali mpya ya Georgia.

Kakha Kaladze baada ya kuwa mwanasiasa
"Nilipotangaza kustaafu kucheza soka, nilisema mechi muhimu zaidi ya maisha yangu ndio imeanza sasa," alisema mlinzi huyo mstaafu mwenye miaka 34 akiongea na shirika la habari la AFP wakati wa kampeni za uchaguzi.

Kampeni za uchaguzi zilizianza kuwa chafu baada ya kituo cha TV cha serikali utoa mikanda ya video ambayo walisema inatoa ushahidi kwamba baadhi wanasiasa, akiwemo Kaladze walikuwa na mahusiano mabosi makundi yanayofanya vitendo vya makosa  - tuhuma ambazo Kaladze aliziita za kijinga. 

“Sina chochote kinachohusiana na Mafia, sio mwanzoni huko nyuma wala sasa," anasema Kaladze.
"Mip[ango yangu kwa sasa ni kutengeneza vizuri barabara na kutoa huduma nzuri za usambazaji wa maji."

No comments:

Post a Comment