Search This Blog

Wednesday, October 10, 2012

AKINA OZIL, GOMEZ NA PODOLSKI WAAHIDIWA €20,000 KWA KILA MECHI MPAKA WATAKAPOFUZU KUCHEZA WORLD CUP 2014

Wachezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani watapokea kiasi cha €20,000 kwa kila mechi ya kufuzu kombe la dunia watakayocheza na ikiwa watafanikiwa kufika nchini Brazil 2014, chama cha soka cha hiyo DFB kimethibitisha.

Kila mchezaji atapata kiasi hicho chote cha fedha kwa kila mechi ya kufuzu, lakini watapokea kiasi hicho mara watakapoweza kufuzu kwenda kwenye michuano ya hiyo ya dunia itakayofanyika nchini Brazil 2014.

"Nina furaha na uharaka na kutokuwepo kwa matatizo katika makubaliano haya. Hii inaonyesha uaminifu uliopo kati ya shirikisho na wachezaji wa timu ya wakubwa ya soka ya Ujerumani," alisema Raisi wa shirikisho hilo Mr.Wolfgang Niersbach.

Ujerumani tayari wameshashinda mechi zao mbili za kundi C na mpaka sasa wanapewa nafasi kubwa ya kuwa viongozi wa kundi hilo  kwa kuongeza pointi 6 nyingine watakapocheza na Irealnd na Sweden Ijuma na Jumanne ijayo.
 

1 comment:

  1. Shafii eeh kila cku "WAHAIDIWA" cyo kiswahili bana..WAAHIDIWA from the word AHADI,rekebisha bana au cyo bro!

    ReplyDelete