Search This Blog

Wednesday, October 24, 2012

MANCHESTER UNITED YASEMA TAYARI TUNA LISTI YA MAKOCHA WATAKAOFAA KUMRITHI FERGUSON

Manchester United leo wamesema kwamba mipango ya kupata mbadala wa Sir Alex Ferguson imeshajadiliwa na mpaka sasa kila kitu kipo tayari lakini mipango hiyo sasa imefungiwa kwenye makabati ya ofisi za klabu hiyo huko Old Trafford.

Makamu mwenyekiti wa Klabu hiyo Ed Woodward amesema kwamba listi ya watakaowania nafasi ya Fergie ipo tayari na wanaijua watu wachache sana lakini hakuna tarehe inayojulikana kuwa ndio itakuwa mwisho wa kocha Mscotland pale Theatre of Dreams.
Alisema: "Tayari tuna mtazamo wa namna mchakato mzima wa kumpata mbadala wa SAF utakavyokuwa na ni aina gani ya mwalimu tunataka na vipi tutampata huyo mwalimu.
Wants it: Jose MourinhoClose to home: David MoyesOut of work: Pep Guardiola



'Lakini kila kitu kuhusu jambo hilo kipo kwenye makabati na mipango yote itakaa huko hata zaidi ya tunavyofikiria."

Majina kama Jose Mourinho na Pep Guardiola, vilevile David Moyes, mara nyingi yamekuw yakihusishwa na kazi ya kumrithi Fergie katika klabu yenye mafanikio kuliko zote pale Uingereza, japokuwa bado haijajulikana lini babu huyo atastaafu.

Akiongea mapema mwaka huu wakati akisherehekea miaka yake yake 25 ndani ya klabu hiyo, babu mwenye miaka 70 alisema: " Sijui ni muda gani nitaweza kuwa hapalakini kama afya yangiu itaniruhusu sidhani kama miaka mingine mitatu au miwli  itakuwa shida.
I'm the boss: United boss Sir Alex Ferguson recently celebrated 25 years at the helm'Nafikiri unahitaji nguvu katika kazi hii. Nimebarikiwa kitu hicho. Nitafahamu wakati utakapofika sifurahii kazi na ikifia hatua hiyo kwa hakika nitastaafu.

No comments:

Post a Comment