Search This Blog

Friday, October 12, 2012

CRISTIANO RONALDO ALIKATALIWA KUSAJILIWA BURE NA OLYMPIQUE LYON

Olympique Lyon ingeweza kumsajili nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo kwa bei sawa na bure, imefahamika. 

Kocha wa wakati huo wa Sporting Lisbon, Laszlo Boloni alitaka kumsajili Tony Vairelles kutoka Lyon kwa kubadilishana na wachezaji wawili akiwamo Ronaldo. 


"Sporting de Portugal hawakuwa na pesa hivyo walipendekeza kubadilishana wachezaji na walikuwa tayari kuwatoa wachezaji wawili, mmoja wao akiwa ni Cristiano Ronaldo, lakini Lyon walikataa ...," alisema Boloni. 


Muda mfupi baadaye Ronaldo akasajiliwa na Manchester United na yaliyobaki yakawa historia.

No comments:

Post a Comment