Search This Blog

Saturday, September 1, 2012

BAHANUZI AIVURUGA COASTAL UNION UWANJA WA TAIFA LEO

 Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima, akimtoka beki wa Coast Union, wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jioni ya leo. 
Katika mchezo huo Yanga imeshinda 2-1, ambapo Coast Union ndiyo walikuwa wa kwanza kuandika bao katika kipindi cha kwanza, ambalo lilidumu hadi kumalizika kwa kipindi cha kwanza na kufanya timu hizo kwenda mapumzi huku Coast ikiwa mbele kwa bao 1-0.
 Kipindi cha pili Yanga ilianza kucheza kwa presha na kasi iliyowachanganya zaidi Coast na kukosa mabao ya wazo na mipira mingine kigonga miamba. 
Alikuwa ni Ally Shamte aliyepiga krosi matata iliyounganishwa moja kwa moja na beki wa Cost, Phillip Kaila, aliyeruka na kuuweka kimiani katika lango lake. bao la pili liliwekwa kimiani na Said Bahanuzi, bao lililodumu hadi kumalizika kwa kipute hicho. 
 Niyonzima, akikwepa kwanja la beki wa Coast Union.
 Joshua (kulia) akimdhibiti Nsa Job wa Coast.
 Kavumbangu, akimiliki mpira mbele ya beki wa Coast.
 Mbuyu Twite, akijiandaa kumimina krosi mbele ya Nsa Job.
Jerry Tegete, akiruka tiktak na kukosa bao...... PICHA na http://sufianimafoto.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment