Search This Blog

Friday, August 3, 2012

TSC MWANZA YAENDELEZA BALAA - UJERUMANI - YAITANDIKA 3-1 NUARBERG NA KUTWAA KOMBE LINGINE

Timu ya kituo cha TSC Mwanza imeendelea kutoa dozi katika michuano mbalimbali inayoshiriki hapa Ujerumani.


Baada ya wiki iliyopita kufanikiwa kutwaa ubingwa wao kwanza tangu waanze ziara yao hapa Ujerumani, kisha kufungwa katika fainali ya kombe Fallerhof kwa penati na FC Basel siku nne zilizopita, siku ya jana klabu hiyo ya academy ya watoto wa mitaani iliyopo jijini Mwanza iliifunga klabu ya Nuarnberg kwa mabao 3-1 katika mechi ya kugombea ya kugombea kikombe cha hisani hapa nchini Ujerumani.


Katika mchezo TSC Mwanza waliwazidi wapinzani katika dakika takribani zote za mchezo na wakafanikiwa kufunga mabao yao yote matatu kupitia kinda lenye hatari mbele ya nyavu Miraji Madenge aka Shevchenko ambaye ni mchezaji wa Simba B.



Shaffih Dauda nikiingia uwanjani kuangalia mechi


No comments:

Post a Comment