Search This Blog

Friday, August 31, 2012

LIVE - SIKU YA MWISHO YA USAJILI BARANI ULAYA - USAJILI ULIOKAMILIKA NA TETESI


Micheal Essien amethibitishwa kuwa ataungana tena na kocha Jose Mourinho, baada ya Chelsea kuthibitisha kwamba atajiunga na Real Madrid kwa mkopo wa mwaka mmoja.


Yossi Benayoun amekamilisha uhamisho wa kujiunga na West Ham kwa mkopo wa mwaka mmoja.


Javi Garcia akiingia kwenye hosptali ya Bridge water kwa ajili ya kufanya vipimo vya afya baada ya klaby yake ya Benfica kukubaliana ada ya uhamisho na City - £16MILLION

Liverpool wamepigwa bao na Tottenham baada ya Clint Dempsey kujiunga na Spurs dakika za mwisho kutoka Fulham kwa ada ya uhamisho wa £6million.

Stephen Mbia yupo Loftus Road akikamilisha vipimo vya afya kwa ajili ya kujiunga na QPR.

Matija Nastasic amekamilisha uhamisho wake kutoka Fiorentina na kujiunga na Mannchester City, na anakuwa mchezaji wa 3 kujiunga na mabingwa hao wa England kwenye siku ya mwisho ya usajili. Wakati huo huo Javi Garcia anafanya vipimo vya afya kwa ajili ya kukamilisha uhamsiho wake kutoka Benfica kwenda City.


Lassana Diara, mchezaji wa zamani wa Chelsea, Arsenal na Portsmouth, amejiunga na Anzhi Makhachkhala kutoka Real Madrid

Breaking news - Edinson Cavan amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea Napoli na kuzima uvumi wa kutaka kujiunga na Chelsea.

Golikipa Hugo Lloris wa Lyon amekamilisha vipimo vya afya na Tottenham na muda mchache na amesaini mkataba wa miaka minne kujiunga klabu hiyo kwa ada ya uhamisho wa £13million.
Nigel De Jong ameondoka rasmi Manchester City na kujiunga na AC Milan kwa ada ya uhamisho ya £3.4million

Gael Kakuta ameenda kwa mkopo Vitesse Arnhem kutokea Chelsea

Ryan Babel mchezaji wa zamani wa Liverpool, amerudi timu yake ya utotoni Ajax akitokea Hoffenheim

Gael Kakuta

Hatimaye Dimitar Berbatov amehamia rasmi Fulham kutoka Manchester United kwa ada ya £5million

Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Douglas Maicon amesajiliwa kutoka Inter Milan kwenda Manchester City

Charlie Adam amejiunga na Stoke City City akitokea Liverpool kwa ada ya £4MILLION



Andy Carroll amejiunga na West Ham kwa mkopo wa mwaka mzima

Rafael Van Der Vaart amejiunga na Schalke akitokea Tottenham Hotspur

Pablo Hernandez amejiunga na Swansea City akitokea Valencia ya Spain

Scott Sinclair amekamilisha uhamisho wake kutoka Swansea na kuhamia kwa mabingwa wa England Man City
ION.

Nicklas Bendtner amehama Arsenal na kwenda kujiunga na Juventus ya Italia

No comments:

Post a Comment