Search This Blog

Friday, July 13, 2012

VICENTE DEL BOSQUE, CARLO ANCELOTTI NA TOP 5 YA MAKOCHA WALIOTIMULIWA KWENYE TIMU ZAO PAMOJA NA KUFANYA KAZI NZURI


1: VICENTE DEL BOSQUE
Real Madrid wana historia ya kubadilisha makocha  wao kuliko wanavyobadilisha vitambaa vya meza za kulia msosi kwenye canteen, lakini kocha wa sasa wa Spain Del Bosque anaweza kuwa ndio aliyefukuzwa kwa kuonewa kuliko wengine. Akiwa ameshinda makombe mawili ya La Liga, mawili ya champions league, Spanish Supercup, UEFA Supercup na Intercontinental cup wakati akiwa kiongozi wa benchi la ufundi la Los Blancos, aliiongoza klabu kupata mafanikio makubwa katika historia ya klabu hiyo.

Mara magalatico wakaanza kuja kwenye klabu bila ruhusa ya kocha, klabu ikafanya uamuzi wa kushtusha zaidi ulipoamua kutomuongeza mkataba mpya  Del Bosque mwaka 2003. Matokeo yake akaondoka na klabu ikashindwa kufanya vizuri hata kufikia kukaa misimu minne bila kombe la maana mpaka mwaka 2007 (chini ya Fabio Capello) pamoja na kutumia mipesa mingi katika kununua wachezaji wakubwa.

Ilikuwa kama wamepigwa laana na Vicente Del Bosque ambaye baada ya kukaa kwa muda bila kazi, mnamo mwaka 2008 baada ya Luis Aragones kujiuzulu kuifundisha Spain - Bosque akatwaa majukumu ya ukocha na kuifanya Spain kuwa moja mataifa ya kuogopwa kwa soka duniani hivi sasa.



2: HARRY REDKNAPP -TOTTENHAM HOTSPUR
Harry Redknapp aliiokoa Spurs kutoka kwenye hali mbaya iliyokuwa ikitishia uwepo wao kwenye ligi kuu  baada ya kocha Juande Ramos alipoiacha klabu ikiwa imepata pointi mbili kwenye mechi nane. Redknapp akaingia White Hart Lane na kuiwezesha timu kumaliza kati kati mwa msimamo wa ligi, kabla ya kuiongoza Spurs kucheza champions league mwaka mmoja baadae ambapo walifanya vizuri kiasi cha kufika kwenye robo fainali.

Ingawa Spurs  walianza vizuri msimu uliopita kiasi cha kuonekana kutishia utawala wa vilabu vya Manchester - lakini mwisho wa siku walimaliza kwenye nafasi ya nne, ambayo walistahili kucheza Champions league kama isingekuwa walioshika nafasi ya sita kutwaa kombe la ulaya mwaka huu. Hili halikumfurahisha Daniel Levy ambaye uhusiano wake na Harry ulianza kuyumba mara baada ya kocha huyo kuanza kuhusishwa na kuchukua nafasi ya ukocha kwenye timu ya taifa ya England, na matokeo yake akamtimua kabisa mwishoni mwa msimu. Andre Villas Boas ndio mwanaume aliyepewa jukumu la kuinoa Spurs - huku akiwa na kivuli cha kuyapita mafanikio ya Harry.


3: SAM ALLARDYCE  - BLACKBURN
Akiwa amefanya maajabu pale Bolton kwa miaka kadhaa iliyopita, Alladyce akapewa jukumu la kuinoa Blackburn. Sam aliweza kujiwekea misingi imara pale Ewood Park, akiiongoza klabu kutoka kwenye matatizo waliyoyapata chini ya Paul Ince , na akafanikiwa kuiweka Blackburn kuwa moja ya vilabu 10 vya juu vya England.

Matajiri wa kihindi "The Venkys' walikuwa na mawazo tofauti, wakamtimua Big Sam mara baada ya kuinunua klabu hiyo na kumpa kazi Steve Keane - mwanaume ambaye bado yupo kibaruani pale Ewood pamoja na kwamba kuteuliwa kwake kumeshadhihirisha kuwa ni moja ya uamuzi mbovu zaidi kwenye historia ya klabu hiyo kwenye Premier league.


4: CARLO ANCELOTTI - CHELSEA
Baada ya kushindwa kumvutia Guus Hiddink kwa dili la moja kwa moja pale Stamford Bridge, Roman Abramovich akaenda na kumpa mkataba wa muda mrefu Carlo Ancelotti kutoka AC Milan. Alimsaini muitaliano huyu mwaka 2009 na akaiongoza vizuri Chelsea kushinda EPL na kombe la ligi mwaka 2010.

Ingawa msimu uliofuatiwa alishinda kombe la FA, lakini alitolewa na Manchester United kwenye Champions league hatua ya robo fainali na kupoteza ubingwa wa ligi kwa United tena. Ancelotti akatimuliwa na kijana mdogo Anfre Villas Boas akapewa nafasi yake lakini nae hakudumu kwa muda mrefu akatimuliwa.

NEIL WARNOCK - QPR
Warnock alifanya kila kitu na kila mbinu na kufanikiwa kuiwezesha timu ya tajiri Tony Fernandes kupanda mpaka ligi kuu ya England msimu uliopita, na kukata kiu ya washabiki wa klabu hiyo kongwe ya kucheza ligi kuu baada ya kushindwa kwa miaka mingi. Ingawa mpaka kufikia kipindi cha Christmas timu ilikuwa hina matokeo mazuri kwenye ligi mmiliki wa timu Tony Fernandes akaamua Warnock aliyewapandisha daraja  hakuwa mtu sahihi wa kuendelea kubaki kwenye benchi la ufundi na hatimaye akamtimua na kumpa kibarua Mark Hughes - badala ya kumpa Warnock fedha za kutosha za kununua wachezaji wenye hadhi na ubora wa kucheza ligi.

Warnock kiukweli hakupaswa kuendewa alivyotendewa na QPR, ukiangalia hakupewa fedha za kutosha kufanyia usajili - ambazo Hughes alipata lakini mwisho wa siku kwa bahati timu ikabakia kwenye ligi siku ya mwisho pamoja na kufungwa na City.

No comments:

Post a Comment