Search This Blog

Thursday, July 5, 2012

JOAO MOUTINHO NA WACHEZAJI WENZAKE WANNE WALIOPANDA THAMANI BAADA YA EURO 2012

Michuano ya Euro 2012 ilikuwa mizuri sana labda uwe muitaliano, na baada ya kuangalia mataifa 16, mechi 31 na magoli 76, Spain wakatawazwa kuwa mabingwa wa ulaya tena.

Wachezaji kama Andres iniesta na Jordi Alba ambao walicheza vizuri sana kwenye mchuano hiyo huku wakicheza kwenye kila mechi, lakini hawakuwa wahispania hao pekee ambao waling'arahuko Poland na Ukraine.

Poland, Russia, Sweden na Denmark wote waliichangamsha michuano hii kwenye hatua ya makundi, lakini pia walikuwa na achezaji ambao walionyesha viwango jinsi vilivyo hatari katika harakati za kusaidia mataifa yao.

Tukiwa nalo hilo kichwani, na ufunguzi wa dirisha la usajili likifunguliwa, hawa ni wachezaji watano - nje ya vikosi vilivyocheza fainali  ambao waliongeza thamani yao kwenye soko la usajili kupitia michuano ya Euro 2012.

ALAN DZAGOEV - KIUNGO MSHAMBULIAJI -URUSI


Akiwa amefunga mabao matatu kwenye hatua za makundi, Alan Dzagoev aljidhihirisha kuwa mmoja ya vijana wadogo wenye future nzuri kwenye soka baada ya kuisadia Russia kupata ilichopta kwenye hatua ya makundi.

Dzagoev, ambaye anaitumikia CSKA Moscow, alianza kufanya balaa kwenye mchezo wa kwanza wa michuano hiyo akiiongoza Russia kuitandika Czech 4-1. Lakini kwa bahati huo ndio ulikuwa ushindi wa mwisho kwa vijana hao kutoka ulaya mashariki.

Alifunga kwenye mchezo dhidi ya Poland ambao uliisha kwa sare ya 1-1 na kuonyesha kiwango kikubwa, alikuwa na control kubwa ya mpira na jicho zuri la kupiga pasi kwenye michezo yote mitatu

Akiwa amebakiza miezi sita kwenye mkataba wake, thamani yake kwenye soko la usajili  haitakuwa kubwa sana kwa sasa. CSKA watafanya kila kitu kuweza kumfunga na mktaba wa muda mrefu.

Ikiwa watafanikiwa, wataweza kupandisha thamani ya mchezaji huyo mpaka kufikia £12million. Ikiwa watashindwa watamuuza kwa bei ya kawaida kuliko inavyopaswa kipindi kijacho cha kiangazi.

THEODOR GEBRE SELASSIE - BEKI WA KULIA - CZECH


Czech Republic walifika robo fainali za Euro, japokuwa walifungwa mabao 4-1 na Urusi, baada ya hapo wakaenda kuwafunga Ugiriki 2-1 na Poland 1-0.

Moja ya sababu kubwa ya kuboreka kwa kiwango chao ilikuwa ni fomu nzuri ya beki wao kulia Theodore Gebre Salassie, ambaye siku kadhaa kabla ya michuano alikubali kuhamia Werder Bremen kutoka Slovan Liberec.

Inaonekana ilikuwa faida kubwa kwa timu hiy ya Bundesiliga kukamilisha uhamisho wa mchezaji huyo kabla ya michuano ya Euro 2012, wakiwa wamelipa $1.6million kwa ajili ya kupata huduma za beki huyo mwenye kukaba na kushambulia kwa kasi.

Kutokana kiwango chake alichokionyesha akiwa Czech, kwa hakika thamani yake ingekuwa imepanda zaidi ya aliyonunuliwa.

Kwa kiwango alichonacho, nguvu na kuwa nautayari wa kusapoti mashambulizi kwenye tatu ya mwisho - Gebre Selassie kwa sasa ana soko kubwa. Kwa hakika akiendelea kuwa hivi alivyo Bremen watapata fedha nzuri sana kama wataamua kumuuza.


ANDRIY YARMOLENKO - WINGA - UKRAINE
Mfumo wa Ukraine wa kiufundi, ulikuwa ume-based. kwenye kushambulia zaidi, kupitia mawinga wao.

Huku winga anyetumia mguu wa kushoto Andriy Yarmolenko akicheza upande wa kulia  na winga anayetumia mguu wa kushoto Yevhen Konoplyanka akicheza winga ya kushoto, Ukraine mara kadhaa walikuwa wakiwatumia mawinga hawa kwenye tatu ya mwisho kutengeneza mipira ya kupiga mashuti ya kupiga krosi.

Huku wachezaji wengi kwa ujumla wakikosa kipaji cha kuchezea mpira kulikuwa kizingiti cha Ukraine kusonga mbele, lakini Yarmolenko, kipekee, alikuwa mchezaji aliyecheza vizuri sana ambaye alionekana muda wowote angeweza kuwadhuru wapinzani.

Akiwa mtulivu alikuwa akiingia katikati kupiga mashuti au kwenda pembeni kuruhusu kutoa sapoti ya kulisha washambulaiji wa kati, Yarmolenko alikuwa mzuri katika kumiliki mpirra na alikuwa mchezaji wa kwanza wachezaji wenzie walikuwa wakimtafuta mara walipopata mpira ili aweze kufanya utundu wake.

Yarmolenko kwa sasa anaichezea Dinamo Kyiv kwenye nchi yake ya ukraine, ambapo huwa anachezeshwa katikati nyuma ya mshambuliaji wa kati. Atakuwa na timu kibao zitakazowatuma mawakala ikiwa taonyesha nia ya kuondoka kwenda kucheza nje ya mipaka ya nchi hiyo.

Kyiv sasa watakuwa wakitegemea ada kubwa ya uhamisho baada ya kiwango alichoonyesha Euro.

JOAO MOUTINHO - KIUNO WA KATI - URENO

Moja kati ya wachezaji wachache kwenye michuano hii wenye uwezo wa kupiga pasi vizuri tu kama ilivyo kwa viungo wa Spain, Joao Moutinho alikuwa nyota iliyoangaza mafanikio ya Ureno kwenye Euro 2012, na ikiwa ataamua kuhama kutoka klabu yake ya sasa ya Porto, atakuwa hajajitendea kitu kibaya kwani kwa hakika atazivutia timu nying sana zenye majina makubwa.

Tofauti na wachezaji wengine kwenye listi hii, Moutinho tayari alikuwa na bei kubwa kabla ya michuano baada ya kucheza vizuri kwa misimu kadhaa akiwa na Porto.

Hivi karibuni kumekuwepo na taarifa za vilabu vya Uingereza Manchester United na Tottenham Hotspur zikiwania saini yake kwenye soko la usajili la hivi sasa 0 huku thamani yake ikitajwa kufikia paundi millioni 32 .

MATS HUMMELS - BEKI WAKATI - UJERUMANI

Hatimaye tumekutana na moja kati wachezaji walioifanya Ujerumani kuwa tishio kwenye michuano ya Euro 2012 - huyu ni beki wa kati Mats Hummels.

Beki huyo wa Borussia Dortmund amekuwa na michuano mizuri. Alizuia kwa kiwango cha juu sana huku hali ya kuweza kuongoza safu ulinzi akionekana kuwa nguvu na ufundi.

Ujerumani wakati wanaingia kwenye michuano hii, safu ya ulinzi ndio iliyoonekana kuwa dhaifu, lakini chini ya ulinzi wa Hummels, Ujerumani walionekana kubadilika na kuwa imara sana kwenye safu ya ulinzi.

Amekuwa akionekana kuwa na thamani ya £20million kwa sasa, Hummels hajaonyesha nia yoyote kuondoka Dortmund, pia klabu yake haijaonyesha nia ya kumuuza.

Ukiangalia kiwango chake kwenye Euro 2012, umri wake na potential aliyonayo huko mbeleni inaonekana kipaji chake kitazidi kukuana kama ikiwa hivyo basi anaweza kuja kuvunja rekodi ya usajili kwa mabeki ambayo kwa sasa inashikiliwana Rio Ferdinand ambayo alisajiliwa na United kwa gharama ya £29million.

No comments:

Post a Comment