Search This Blog

Thursday, July 12, 2012

EXCLUSIVE: EMMANUEL OKWI SASA KWENDA AUSTRIA JUMAPILI HII - PARMA MMMMH!??? AIOMBEA SIMBA USHINDI DHIDI YA AZAM LEO

Dakika chache zilizopita nimetoka kufanya mazungumzo ya simu na mshambuliaji wa klabu ya Simba na timu ya taifa ya Uganda the 'Cranes' Emmanuel Okwi kuhusu sakata la uhamisho wake kwenda barani ulaya kufanya majaribio ya kujiunga na moja ya vilabu vikubwa kwenye bara hilo.

Kwenye mazungumzo yetu yapatayo dakika tatu, Okwi kwanza alinitaka niwaambie mashabiki wa Simba kwamba anaiombea kheri klabu yake kwenye mchezo wa fainali ya leo usiku dhidi ya Azam FC ili kuweza kuanza msimu mpya vizuri, pili ndio akanipa taarifa juu ya sakata lake la kutafuta timu ya kucheza ulaya, "Shaffih nashukuru mungu leo nimepata viza ya kwenda nchini Austria kwenda kufanya majaribio na klabu Redbull Salsburg inayoshiriki ligi kuu ya Austria. Jumapili ya wiki hii ndio nategemea kuondoka rasmi Uganda na kwenda huko kufanya majaribio. Taarifa nyingine nitaendelea kukupa nikiwa huko."

Okwi ambaye wiki iliyopita ilisemekana alikuwa akitafuta viza ya kwenda nchini Italia kwenda kufanya majaribio na klabu ya Parma baada ya kukataa kujiunga na vilabu vikubwa vya South Africa Orlando Pirates na Mamelodi Sundowns - amesema mpango huo lakini kwa sababu tofauti zilizo nje ya uwezo kwa sasa zimembidi aende Austria kwanza."

Redbull Salsburg ni klabu inayomilikiwa na kampuni ya utengenezaji vinywaji ya Redbull. Ni bingwa wa mara saba wa Austria Bundesiliga pia ni moja ya vilabu vikubwa barani ulaya vyenye academy za soka barani Afrika - ikiwa yenyewe imejenga shule yake ya kukuza vipaji vya soka nchini Ghana.

3 comments:

  1. Mi ni shabiki wa YANGA lakini nakuombea lila la heri Okwi,kwa kipaji chako naamini kokote unaweza cheza soka.

    ReplyDelete
  2. Namuomba kama akishindwa majaribio yake arudi haraka katika klabu yake ya simba ili aendeleze makali yake.

    ReplyDelete
  3. nauomba Okwi kamaa akishindwa majaribio yake arudi simba na sio yanga kama wengi wanavyodai

    ReplyDelete