Search This Blog

Thursday, June 7, 2012

UFARANSA: HAIJASHINDA MECHI YOYOTE KWENYE EURO WALA WORLD CUP TANGU 2006: ITAFANYA NINI KWENYE EURO 2012.

Laurent Blanc anaichukua Ufaransa kwenda nayo kwenye Euro 2012 huku akiiongoza timu hiyo kutofungwa katika michezo 20, ambayo inahusisha ushindi dhidi ya Ujerumani, England na Brazil. Lakini kocha huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa bado haipi nafasi kubwa timu. Ufaransa haijashinda mechi yoyote ya mwisho ya michuano mikubwa yenyewe tangu mechi ya nusu fainali ya World Cup 2006 (haikushinda mechi yoyote kwenye Euro 2008 na WOZA 2010), huku wakishika nafasi ya 16, nafasi tisa nyuma ya wapinzani wao England wanaoshika nafasi ya saba kwenye ubora wa viwango wa FIFA.

Blanc bado na maumivu ya kichwa kuhusu upangaji wa kikosi hasa kwenye nafasi ya beki wa kushoto, ambapo Gael Clichy ameonyesha kiwango kizuri kwenye mchi dhidi ya Serbia siku chache baada ya Evra kucheza chini kiwango dhidi ya Iceland. Kiungo mkabaji Yann M'Vila pia ana majeruhi ya enka ambayo yatamfanya asicheze mchezo wa kwanza na Alou Diarra anategemewa kumbadili.

Lakini hiki ni kikosi tofauti sana na kile kilichoenda kwenye kombe la dunia 2010 chini Raymond Domenech nchini South Africa. Golikipa Hugo Lloris sasa ni nahodha, lakini Phillipe Mexes, M'Vila na Karim Benzema ambaye yupo kwenye form sasa hivi, wote waliikosa michuano ya WOZA 2010 hivyo hawakuwemo kwenye aibu iliyopita. Lakini hili haliwezi kusemwa linapojitokeza jina la Frank Ribery, ambaye kwa sasa yupo desparate kuweza kurudisa imani na upendo wa wafaransa. Baada ya miaka 3 bila kufunga bao, Ribery alifunga mara mbili katika mechi 2 za kirafiki zilizopita. Ikiwa ataanza japo kuileta nusu ya uwezo anaonyesha Bayern Munich akiwa kwenye jezi za Blue, then Les Bleus wanaweza kuwashangaza wengi.

WACHEZAJI MUHIMU

Karim Benzema
Tumaini kubwa la soka la Ufaransa lilikuwa na mwanzo mmbaya kwenye career yake ndani ya timu ya taifa ya Ufaransa kwenye michuano ya Euro 2008, pale alipotuhumiwa kwa pamaja na Samir Nasri kwa kutokuwa na heshima kwa wachezaji wakubwa na kwa kutompasia mipra mingi Thierry Henry. Akaachwa kwenye kombe la dunia 2010, lakini amekuwa ndio mfungaji bora wa Ufaransa chini ya Blanc, akifunga mabao matano katika mechi 17, likiwemo goli la ushindi dhidi ya Brazil. Huku akiwa amemaliza msimu wa mafanikio na Real Madrid akifunga mabao 32, huku akitamba kwamba amekuwa mchezaji mzuri zaidichini Jose Mourinho. Na kama hayo maneno yataonekana kwenye vitendo basii Ufaransa itaifadika sana.


Samir Nasri
Mpaka aliposhinda kombe la premier league na Manchester City mwezi uliopita, Nasri alikuwa ameshinda kombe moja tu kwenye maisha yake ya soka la kulipwa: alipofunga goli la ushindi kwenye fainali ya Euro 2004 kwa timu ya vijana wa miaka 17. Nasri ni moja ya sehemu ya kundi 'Kizai cha 87' kinachowahusisha wachezaji waliozaliwa mwaka 1987 na kwa sasa wakiwa ndio wanaelekea kwenye vilele vya viwango vyao wakiwa kwenye timu ya taifa ya wakubwa. Kundi hilo lilikuwa linawahusisha Benzema, Hatem Ben Arfa, Jelemu Menez na Blaise Matuidi - wote walicheza kwenye Euro 2004, na sasa wapo kwenye Euro 2012 ya wakubwa. Kama kiungo mchezeshaji Nasri anayo nafasi ya kuifanya timu ikacheza soka zuri la kushambulia na ahatimaye kuiletea timu ushindi. Ni jukumu ambalo amekuwa alilitumikia siku nyingi, sasa hivi anayo nafasi ya kuonyesha kama kweli anastahili.

Yann M'Vila
Kiungo mkabaji anatarajiwa kuuzwa kwa mapesa mengi mara baada ya michuano hii, na klabu yake. Rennes, inaweza ikataka kuongeza beikama atacheza vizuri kwenye Euro.M'Vila alikuwa na bahati kuikosa world cup, alitoswa na Domenech lakinii chini ya Blanc amejihakikishia nafasi ya kudumu. Akiwa na miaka 21, amekuja kuwa mchezaji muhimu wa Ufaransana kwa jinsi inavyocheza, kuvunja mashambulizi ya wapinzani na kushambulia kutokea kwenye kiungo huku akiwa na uwezo mkubwa wa kupiga pasi. Ameshajulikana kwamba ataikosa mechi yake ya kwanza ya Euro dhidi ya England na anategemewa kurudi dimbani kwenye mechi ya Ukraine.

No comments:

Post a Comment