Search This Blog

Saturday, June 23, 2012

OKWI AGEUKA LULU SOKO LA USAJILI: SASA TIMU MOJA YA SERIE A NA MAMELODI SUNDOWNS ZAGOMBEA SAINI YAKE

Nyota ya mshambuliaji wa kimataifa wa Simba raia wa Uganda Emmanuel Okwi, inazidi kuwaka, siku chache baada ya klabu bingwa ya Orlando Pirates kutuma barua ya kumtaka mshambuliaji huyo wa Simba aende kufanya majaribio kwenye klabu hiyo, leo hii timu pinzani ya Orlando kwenye ligi ya Afrika kusini, Mamelodi Sundowns wameuambia uongozi wa Simba kwamba wapo tayari kumnunua mshambuliaji huyo.

Taarifa zilizothibitishwa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinasema kwamba Mamelodi wametuma maombi ya kutaka kumsaini Okwi ambaye amekuwa na msimu mzuri sana ndani na nje ya ligi kuu ya Vodacom msimu ulioisha.

Pia chanzo changu hicho cha habari kutoka ndani ya Simba kilisema kwamba kuna timu moja inayoshiriki ligi kuu ya Italia Serie A, wameonyesha nia ya kumtaka Okwi lakini wamesema kwamba wanasubiri mpaka michuano ya Euro itakapoisha ndipo watakapoamua juu ya suala la usajili wa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uganda.

21 comments:

  1. Shaffih huko simba ndio kwako,yaani unastahili kuwa msemaji wao

    ReplyDelete
  2. kaka!!!! kuna ubaya gani kwa habari hiyo? au roho in akuuma? na kama inakuuma okwi kwenda huko kwa sababu zipi? acha roho mbaya haya maisha tu? kama unataka na wewe kacheze soka? si kila mahali unaleta uyanga. fikiria kwanini asiwe mtanzania? tunakosea wapi sisi?

    ReplyDelete
  3. watu wengine bwana! sasa hapo Shafii kakosea nini? kwanini mnapenda kumlaumu mtu hata bila kosa? Sasa Shafii anahusika na usemaji wa Simba? Hii ni blog na inaripoti habari za michezo bila kujali ni habari ya timu gani.

    Ifikie kipindi tuwe na staha kwa watu mbali mbali na kuheshimu taaluma ya mtu. Si ajabu nyie ndiyo mnaomtuma mzee Akilimali kuvuruga Yanga.

    Okangi.

    ReplyDelete
  4. I thnk kila habari ya simba ikiwekwa hapa ni unazi!basi shaffih usiwe unaeka habari za simba apa.weka tu simba ikifungwa na YANGA.

    ReplyDelete
  5. Kuna watu majuha kabisa,unachukia mtu akitaka kufanikiwa?yaani hata nikikuita bwege nitakuwa nakusifia.All the best Okwi.

    ReplyDelete
  6. Uelewa mdogo...@Okwiii akifanya vzr anaitangaza tz na east afrika kisoka
    acha UyangeeYange Ji2 zima uooni hata Aibuuu

    ReplyDelete
  7. Tanzania bado sana! Huyo jamaa anayemlalamikia Shaffih nadhani bado sana na atakuwa mwanakjj. Jamaa abadilike awe up to date! Hatembelei blogs za wenzetu majuu? Shaffi usichoke kutuhabarisha. Hao wenye Majungu huwa hawakosekani. Keep it up Shaffih, watatokea akina AKILI mali wengi sana, usitingishwe nao!

    ReplyDelete
  8. Kweli nyinyi watu ya yanga akili zenu zinafanana na waendesha madaladala sasa shaffih kakosea nini kutoa habari hiyo? Mbona jana katoa picha za yondan akiwa mazoezini kaunda mpaka video yake hamjaongea chochote?

    ReplyDelete
  9. hakika hakuna tusi linalofaa kuwatukana washabiki wapuuzi wa aina hii, nini hasa alichokosea shaffih? mmewekewa mpaka picha ya kelvin yondan akiwa mazoezini kaunda, jee shaffih ni yanga? alishaweka picha ya kiggi makasi akiwa mazoezini simba? ama hakika wafadhilaka wa pundaka. sijui mijitu ya ajabu imetokea wapi miaka hii? halafu wanakufa watu wa maana lakini mishenzi ambayo ipo kwa ajili ya kuwakera watu wengine ndio inaendelea kuishi.

    ReplyDelete
  10. uelewa mdogo elimu finyu mawazo mgando ndo fikra za huyo jamaa hapo juu. shaffih kakosea nn hapo? au umetumwa? blog ziko nyingi si lazima upate habari hapa. kama vp tembeleeni ile yenu iliyojaa unazi BIN nn sijui..

    ReplyDelete
  11. kaka shsaffir...usikatishwe tamaa na watu wenye ALTITUDE ndogo....Fanya kazi...hawa watu wenye akili ka ya Akilimali...achana nao..Bro fanya kazi..Okwi Deserves kuchezaa hata Arsenal...kunawatu pale Go our Boy! God Bless you bro....Bravo Simba Bravo Tanzania Bravo Uganda and East Africa.....

    ReplyDelete
  12. Nimeamini kuna watu mafala duniani,mbona me sijaona kosa alilo fanya shaffih hapa,hii si habari ya michezo kama habari zingine jamani!.

    ReplyDelete
  13. Kaka Shaffih kaza uzi ata yesu alisemwa vibaya lakini alisonga mbele we achananao endelea kutupa habari wadau wa soka tuache uyanga Okwi anastahili kuchezea ata man united viva Shaffih..............

    ReplyDelete
  14. kwanza kwenye team kuwa na shabiki kama huyo ni hatari sana coz hakili zake ni finyu swala la uyanga linakujaje sasa na ndio maana yanashindwa kuuza wachezaji nje kwasababu ya majungu hakili zao zote zimetekwa na mzee akilimali wao muda wote wanamsikiliza yeye hata kama anawaposha wenyewe hastuki sasa team hiyo inauzwa kwa wahindi.

    ReplyDelete
  15. ndo matatizo ya wna yanga hayo maana kwa hivi karbun et waliona wakimchukua kaseja wataua simba na bado ikaendelea kuwa juu. Haya kipigo cha 5 bila hicho, wanaona kwamb the solution ya kuiua simba ni kumsajil yondan. Ama kwel hawa n majuha kwel, siklzen nyie yang simb kisma cha wachezaj 2natengeneza vijana na kuwakuza na hatuna time na yondan but 2nchotaka taratibu zifuatwe na kwa tarifa yenu shomar kapombe ndo kisik cha baadae.

    ReplyDelete
  16. Mwache ndala aongee mana wao mchezaj akiuzwa mbali sana kule kwa wauza lamba lamba,,unafkr haogaop aliondoka henry,mgosi,samata,mrwanda,,santo na bdo walikula tano,akiondoka okwi je,,uchaguz utasitishwa kwanza wajadiliane simba inajiamin nn kuuza wachezaj tegemeo

    ReplyDelete
  17. Sasa Shaffih akisema ukweli kuna ubaya gani wanafiki wa soka utawajua tu wanataka waambiwe wanayotaka. Shaffih you are doing good job in Tanzanian football go ahead brother

    ReplyDelete
  18. Nyie kosa la shaffih kwa ndala hamjaliona kumbe,,kosa lake kusema kuna timu serie A inamtaka,,wao waltaka wasikie kuna tmu india na thailand znamtaka,apo shaffih angekuwa hana makosa.

    ReplyDelete
  19. Miyanga bwana,yaani akili zao mgando mpaka basi.cjui hata ni lini watakuwa na akili za maendeleo.wote ni Akilimali type...

    ReplyDelete
  20. shaffih kuna taarifa zimeanza kuzagaa kuwa yanga wanataka kuibomoa simba tena kwa kumsajili kapombe kimya kimya eti kwa vile hana jina kubwa simba na kiwango chake kikubwa zina ukweli ndani yake?

    ReplyDelete
  21. tajiri wao manji ataibomoa yanga hata azamu kwa pesa yake hatima yake ni kuua mpira wa tz chunga sana

    ReplyDelete