Search This Blog

Saturday, June 9, 2012

EURO 2012: UHOLANZI VS DENMARK - SAFU BORA YA USHAMBULIAJI DHIDI YA TIMU ISIYOTABIRIKA.

Netherlands-Denmark

VIKOSI VINAVYOWEZA KUANZA
Uholanzi: 1: Stekelenburg 2: Wiel 3: Bouma 4: Heitinga 5: Vlaar 6: De Jong 7: Robben 8: Van Bommel 9: Van Persie 10: Sneijder 11: Afellay

Denmark: 1: Lindergaard 2: Wass 3: Poulsen 4: Kjear 5: Agger 6: Poulsen 7: Rhommedal 8: Kvist 9: Bendtner 10: Erikssen 11: Kron-Dehli

MAMBO MUHIMU KUHUSU MECHI
  • Kumekuwepo na tetesi kwa wiki kadhaa kuelekea Euro 2012 kuhusu kama meneja wa Uholanzi Bert van Marwijk atawachezesha  washambuliaji  wake wawili Klaas-Jan Huntelaar na Robin van Persie, pamoja kupenda kutumia mfumo wa 4-2-3-1 katika kufuzu, van Persie alikuwa akichezeshwa upande wa kulia lakini amekuwa akicheza pekee yake mbele katika mechi za kirafiki za hivi karibuni ikiwemo mechi waliowafunga Ireland mabao 6-0.
  • Ibrahim Afellay pia alicheza vizuri kwenye mechi hiyo, akifunga bao zuri na akiongeza lingine kwa penati. Anaweza kuanza kwenye mchezo wa leo kama kocha ataamua kutumia mfumo wa kushambulia zaidi, akimuacha Van Marwijk akiwa na machaguo mengi kwenye benchi, huku Huntelaar, van der Vaart na Kuyt pia wakiwa na nafasi ya kuanza.
  • Joris Mathijsen pia ana wasiwasi wa kucheza kwenye mchezo wa ufunguzi kwa majeruhi aliyoyapata wiki iliyopita. 
  • Wilfred Bouma anahangaika kuweza kuimudu nafasi ya beki wa kushoto huku vijana Jetro Willems na Stijn Schaars wakiwa wameonyesha viwango vizuri.
  •   Denmark
  • Denmark hawana majeruhi mpya kwenye kikosi, lakini kuna maswali mengi juu ya nani anapaswa kuanza kwenye kikosi.
  • Chistian Poulsen hakuanza katika mechi dhidi ya Australia wiki iliyopita na Niki Zimling anaweza akaanza tena.
  • Pia kumekuwepo na na wasiwasi kuhusu kiwango cha Christian Eriksen, lakini pia kumekuwepo na waiwasi kidogo juu ya nafasi yake ndani ya kikosi lakini uwezo wake na ubunifu ni kitu ambacho Denmark wanahitaji.
  • Wass na Lars Jacobsen wapo kwenye upinzani wa nafasi ya beki wa kulia.

TAKWIMU
Denmark wameshinda mechi zao 4 za mwisho za Euro Cup.

Uholanzi wamekuwa wakifunga mabao atleast mawili katika mechi 6 kati ya saba za mwisho za kombe la Euro.

Denmark  wamekuwa wakifunga mabao atleast mawili katika mechi 4  za mwisho za kombe la Euro.

1 comment:

  1. mtu kesha gongwa biashara imekwisha ndio soccer

    ReplyDelete