Search This Blog

Saturday, June 30, 2012

ANDRE VILLAS BOAS KUZIKOSA ZAIDI YA BILLIONI 20 ZA CHELSEA IKIWA ATAKUWA KOCHA WA TOTTENHAM WIKI IJAYO

Andre Villas Boas atapoteza kiasi kinachokaribia £11million wakati atakapotangazwa kuwa kocha mpya wa Tottenham wiki ijayo.

Mreno huyo, 34, hakupokea fidia yote kwa pamoja ya kuvunjika kwa mataba wake alipofukuzwa na Chelsea mwezi wa tatu mwaka huu, ikiwa ni miezi nane tu tangu aliposainishwa mkataba wa miaka 3.

Badala yake, Chelsea walikubaliana na AVB kuendelea kumlipa msharaha wake wa kawaida wa £100,000 kwa wiki mpaka pale atakapopata kazi mpya.

Mpaka sasa ameshapokea mshara wa miezi mitatu tangu kuanza mpaka mwishoni mwa mwezi huu.

Lakini ikiwa atakuwa kocha wa bosi wa White Hart Lane, Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich ataachana na mpango wa kumlipa mshahara AVB, na kocha huyo atapoteza mkwanja wa malipo ya miezi 25 iliyobaki yenye thamani ya £10.8million.

Ripoti kutoka nchini Ureno zinasema kwamba mazungumzo kati ya AVB na Spurs yamekwamia kwenye suala la fedha.

No comments:

Post a Comment