Search This Blog

Saturday, May 12, 2012

UMRI WANGU HAUNIRUHUSU TENA KUCHEZA SOKA LA ULAYA - NESTA ATOA SABABU ZA KUONDOKA AC MILAN.

Katika kizazi cha dhahabu cha soka la kushambulia, ambapo wachezaji wawili wanaweza kufunga magoli nusu karne ndani ya msimu mmoja, muda mwingine ni rahisi sana kusahau kwamba kuna wachezaji wengine wenye ujuzi wanaocheza katika eneo lingine la uwanja ambao kazi yao ni kuwazuia

Mmmoja wao ni Alessandro Nesta, beki mwenye halisi kabisa aliyebarikiwa uwezo mkubwa wa kukaba ambaye akiwa na miaka 36 sasa ameamua kuacha kucheza soka la Seria A.

Alipewa ofa ya mkataba mpya na Milan, Nesta akakataa, akisema kwamba hana tena uwezo uwezo wa kuendelea kucheza soka la level ya kwanza.

"Mchezo wa kasi ya juu ya soka la Italia, champions league na Italian Cup unamaanisha kwamba kwa umri wangu sitoweza kucheza muda wote, Na mimi sio mtu wa kukubali kukaa na kusubiri kwenye benchi."

Hivyo ni wapi panamfaa mchezaji huyu ambaye anakiri sasa umri unamtupa mkono? MLS - ligi ya Marekani.

Alipoulizwa kuhusu kuhusishwa na kujiunga na New York Red Bulls, Nesta akakiri: "Nitaenda kwa moyo mmoja, ningependa kwenda kucheza huko lakini mpaka sasa hakuna kilichosainiwa, na pia kuna nafasi nyingine zimejitokeza kwa ajili yangu.
 

1 comment:

  1. Alesandro Nesta tam mic saaana... beki mstaarabu...

    ReplyDelete