Search This Blog

Saturday, May 19, 2012

MTANZANIA MULUMBU:CHELSEA WANA NAFASI KUBWA YA KUBEBA KOMBE LEO -ATOA USHAURI KWA WABONGO


Leo nimekutana mtanzania bwana Mulumbu ambaye nimepiga nae story tofauti kuelekea mechi ya leo usiku.


Shafih: Unauzungumziaje mchezo wa leo usiku kati ya Bayern vs Chelsea?



Mulumbu: Mchezo utakuwa mgumu sana lakini naipa nafasi Chelsea kwa sababu Bayern wana tataizo la defense, wanawakosa mabeki wao muhimu kama akina Alaba ambao wana uzoefu kiasi, pia waliopo kama replacement bado hawana uzoefu wa kupambana na deadly strikers kama Didier Drogba na Fernando Torres.



Shaffih: Chelsea nao watawakosa wachezaji wao muhimu kama John Terry, Ramirez na Meireles, huoni kama na wenyewe wana pengo kubwa?

Mulumbu: Utofauti kati ya Bayern na Chelsea kwa wachezaji, ni kwamba atleast kwa Chelsea wabadala kama wa akina Terry wana uzoefu, mtu kama Essien kila mtu anafahamu uwezo wake na uzoefu, David Luiz na Gary Cahil wamecheza kwenye level ya juu kwa muda mrefu sasa. Halfu kitu kingine Chelsea wataingia kwenye mchezo wakiwa wana presha ndogo sana ukiwafananisha na Bayern, hivyo hiyo ni advantage nyingine kwao.

Shaffih: Tangu nifike hapa nimegundua kwamba mashabiki wengi wa hapa wanaonekana kutoisapoti Bayern. Hii ni kwanini?

Mulumbu: Hapa Munich mashabiki wamegawanyika kutokana na timu zilizopo hapa, kama ilivyo nyumbani pale Dar es Salaam Uyanga na Usimba, na hapa kuna timu mbili kubwa Bayern na TSV 1860 Munich - hivyo kwa mtazamo mashabiki wengi wa hapa ni wa timu ya TSV 1860 na ndio maana unaona hali hiyo.


Shaffih: Unazungumziaje soka la nyumbani na ushauri kwa watanzania.
                             

No comments:

Post a Comment