Search This Blog

Saturday, May 19, 2012

FAINALI YA MABINGWA WA ULAYA: TIKETI ZAPANDA MPAKA EURO 1500 -2500 ZA KIBONGO NA BADO ZAKOSEKANA

Football is business.......
Wakati jana nafika hapa Munich tiketi za mchezo wa fainali ambazo kwa jana tu zilikuwa zikipatikana kwa taabu, leo zimepanda bei maradufu kutoka Euro 1500 kwa jana mpaka EURO 2500 leo hii. 

Katika hali ya kushangaza pia tiketi hizo za EURO 2500 ambazo kwa haraka haraka ni kama shilingi millioni 4 za kitanzania, nazo zimeisha hivyo kusababisha uongozi wa jiji la Munich pamoja UEFA kuchagua sehemu maalum ambazo zimetengenezwa na kuwekwa Big screens.


Sehemu hizo pia nazo zimejaa na kuwa sold out kwa maana tiketi zote nazo zimeisha. Kwenye mabaa na pub nyingine nyingi hapa Munich ambazo huonyesha mipira napo kumekuwa sold out. Ni watu wengi inaonekana watakosa nafasi ya kuangalia mechi hii uwanjani.
Huyu mzungu ni mmarekani ambaye amesafiri kutoka Califonia kuja kuangalia fainali lakini amekosa tiketi.

 Kwa mfano nikiwa kwenye matembezi yangu leo nilikutana na Jamaa mmoja raia wa Marekani ambaye ambaye amesafiri kutoka Califonia mpaka Munich lakini maskini ya mungu amekosa tiketi.  


Kiukweli mpaka sasa kila sehemu ni Champions league final ndio kitu kinachotawala. Nimejifunza namna wenzetu wanavyoandaa matukio ya kuyafanyia promotions ya kutosha na ndio maana ni vigumu kwa matukio yao kufeli na mwisho ndio maana wanakuwa wanafanya biashara kubwa na kuwa matajiri.

No comments:

Post a Comment