Search This Blog

Saturday, April 21, 2012

BARCELONA VS REAL MADRID: MATUKIO MUHIMU KATIKA HISTORIA YA EL CLASICO

Muda umekaribia tena kwa mara nyingine! El classico nyingine hii hapa ndani ya wikiendi hii.

Mtanange mkali kati ya Barcelona na Real Madrid siku zote umekuwa ukileta hisia tofauti na raha kwa mashabiki wa soka ulimwenguni, matukio ya kutatanisha na ya kukumbukwa zaidi. Kesho Jumamosi pale Nou Campkutaweka moto mkubwa sana, pamoja tu na hali ya upinzani kati ya timu hizi mbili lakini mchezo huu unaongezewa utamu kwa kuwa unaweza ukaamua nani awe bingwa wa La Liga.

Wamekutana karibia mara 200 na ndani ya kipindi cha miaka 100, kila kitu kutoka katika mpambano kimekuwa kikotoa matukio ya ushindani wa hali juu pindi vigogo hawa wawili wanapokutana.

Ebu leo tujikumbushe baadhi ya matukio mengi ya kukumbukwa katika El Classico.


KURUDI KWA ABIDAL BAADA YA OPERATION

Eric Abidal, ambaye ka sasa anaendelea kujiuguza baada ya kufanyiwa ubadilishwaji wa ini, mwezi Machi 2011 alifanyiwa upasuaji wa ini. Alirudi uwanjani na kucheza mechi yake ya kwanza baada ya operesheni katika mechi dhidi ya Real Madrid katika champions league  semi final.


KUSHANGILIWA KWA RONALDINHO @BERNABEU

Baada ya kuwatesa Real Madrid katika mechi ambayo Barca waliwafunga wapinzani goli 3-0, wakati mbrazili huyo alipofunga mabo mawili katika uwanja wa Bernabeu mjini Madrid - Na mechi ilipoisha akiwa mashabiki wote uwanja mzima waliinuka kumshangilia.


GOLI LA KWANZA LA CRISTIANO RONALDO DHIDI YA BARCA

Baada ya kucheza mara sita dhidi ya Barca, na kufeli kuwafunga, Cristiano Ronaldo hatimaye alifanikiwa kuwafunga Barcelona kwa mara ya kwanza mwezi wa April 16, 2011 katika suluhu ya 1-1 katika uwanja wa Santiago Bernabeu. Tangu wakati huo mpaka leo tayari ameshawafunga Barca mabao manne likiwemo la ushindi katika mechi ya fainali ya kombe la mfalme.   



USHINDI WA 11-1

 Ushindi mkubwa zaid kuwahi kutokea katika  El Classico, ulikuwa ushindi wa 11-1 wa Real Madrid dhidi ya Barca katika mchezo wa pili wa nusu fainali ya pili ya Copa del Deneralisimo ambalo la sasa linaitwa Copa del Rey mwaka 1943. Real walifungwa na Barca 3-0 katika ngwe ya kwanza.


USAJILI WA KWANZA WA KUTOKA BARCA KWENDA MADRID

Mwezi May 1902, Alfonso Albeniz alikuwa mchezaji wa kwanza kuweka rekodi ya kuhama kutoka Barcelona na kujiunga na Madrid. Luciano Lizarraga nae alikuwa mchezaji wa kwanza kuondoka Madrid kwenda Barca. in 1905.


REKODI YA UFUNGAJI WA MAGOLI

Huku wakiwa wameshafunga mabao 107 katika La Liga msimu huu msimu huu, Madrid wanahitaji goli moja tu kuweka rekodi ya klabu na ligi kwa kufunga magoli mengi katika msimu mmoja. Barcelona wenyewe wana rekodi ya kufunga mabao 105, kwa sasa wameshafunga mabao 96. Huku pia Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wameshaweka rekodi zao binafsi ya kufunga mabao mengi katika La Liga wikiendi iliyopita walipoweza kufunga magoli 41 msimu huu.


MADRID WANAONGOZA KWA KUIFUNGA BARCA

Barcelona na Madrid wameshakutana mara 217 katika mashindano yote. Madrid kwa sasa ndio wanaoongoza kwa kuwafunga wapinzani wao wakiwa wameshinda mechi 86, wakati Barca wakiwa wameshinda 85. Katika La liga pekee Los Blancos wameshinda 68 wakati Catalans wameshinda 64.H | Head-To-Head advantage to RealH | Head-To-Head advantage to Real

JOHAN CRUYFF NA DRAM TEAM YAKE
Johan Cruyff akiwa na kikosi chake maarufu cha Dream Team aliweza kuwafunga Real Madrid goli 5-0. In 1973 akiwa mchezaji , aliisadia Barca kuifunga 5-0 Real @Santiago Bernebau, na baadae akiwa kocha wa The Dream Team ya Barca aliiongoza La Blaugurana kuwafunga tena Madrid  5-0 pale Nou Camp, lakini nae akapokea kipigo cha idadi hiyo hiyo mwaka 1995 mjini Madrid.


GOLI LA MAPEMA ZAIDI YA BENZEMA.

Katika mechi ya mwisho ya wapinzani hawa mwezi December 10, 2011, Karim Benzema alifunga goli la mapema zaidi katika historia ya El Clasico alipofunga goli sekunde ya 22 ya mchezo.


MICHEAL LAUDRUP NA REKODI ZAKE

Michael Laudrup sio tu kwamba aliwahi kuizchezea timu hizi mbili zote lakini pia alihusika na kuwa katika ushindi wa 5-0 kwa timu zote mbili. Aliwasaidia Barca kuwafunga Madrid kwa idadi hiyo mwaka 1994, lakini msimu uliofuata akiwa upande wa Madrid. Pia ndiye mchezaji pekee kuweza kushinda makombe matano ya la liga kwa mfululizo akiwa na klabu mbili tofauti.


MESSI NA REKODI YA CESAR RODRIGUEZ

Lionel Messi hivi karibuni alivunja rekodi ya Cesar Rodriguez iliyokaa muda mrefu kama mfungaji bora wa muda wote wa katika historia ya Barcelona, katika mechi rasmi, lakini bado anaikimbiza rekodi nyingine ya kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi katika El Clasico, Rodriguez alifunga mabao 14 dhidi ya Madrid - 12 kwenye La Liga na mawili katika Copa del Rey, wakati Messi ameshafunga 13 - nane katika La liga, matatu katika Spanish Supercopa na mawili katika Champions league.

SARE TASA

Katika mechi 217, ni mechi nane tu ambazo ziliisha kwa sare tasa ya 0-0. Mechi hizi zote ni la liga. Na ilikuwa mwaka 1973 ambapo kulikuwa na mechi za mfululizo zilizoisha kwa sare tasa.



KICHWA CHA NGURUWE

Ingawa wachezaji 26 walishatoka klabu moja na kwenda nyingine kati ya Barca na Madrid, lakini uhamisho wa Figo kwenda Madrid kutoka Barca ulileta utata mkubwa. Aliporudi Nou Camp kwa mara ya kwanza in 2002, mreno huyo alitupiwa kila aina ya kitu kilichokuwepo karibu na mashabiki - kikiwemo kichwa cha Nguruwe huku akiitwa Judas.

KUTOLEWA KATIKA MICHUANO YA ULAYA

Barcelona ndio ilikuwa timu ya kwanza kuitoa Madrid katika kombe la ulaya pindi Wakatalunya walipomaliza utawala wa miaka mitano wa Madrid kama Mabingwa wa ulaya kutoka 1961-61 kwa kuwafunga Real katika raundi ya kwanza na kuwatoa kwa idadi ya 4-3.


REKODI YA RAUL DHIDI YA BARCA

Raul ni mfungaji namba mbili katika listi ya wafungaji bora wa Clasico nyuma ya Di Stefanoakiwa amefunga mabao 15 - 11 kwenye La Liga, 3 mkatika Spanish supercopa na moja katika UCL. Cesar Rodriguez, Gento, na Ferenc Puskas wote wana mabao 14.


MOURINHO VS GUARDIOLA


Rekodi ya Jose Mourinho (akiwa na Inter, Chelsea na Madrid dhidi ya Barca inaonyesha ameshinda mechi nne, droo 7 na vipigo 9, huku timu zake zikgunga mabao 24 na kufungwa mabao 34. Pep Guardiola rekodiyake dhidi ya Real, inayonyesha ameshinda mara 9, droo nne na kufungwa moja.



VALDES VS CASILLAS

Barcelona keeper Victor Valdes ameshinda tuzo ya Zamora mara nne, na sasa yupo nyuma kwa kwa ushindi mmoja kuifikia rekodi ya Antoni Ramallets. Iker Casillas ameshinda tuzo hiyo mara moja tu. Mbele ya mchezo wa kesho - Valdes tayari ameshafungwa mabao 23 katika mechi 32, wakati Casilas amefungwa mabao 29 katika mechi 33.


MADRID NA UKAME WA KUIFUNGA BARCA KWENYE LA LIGA


Madrid hawajafanikiwa kuwafunga Barcelona katika La Liga katika mechi 14 ndani ya dakika 90.


XAVI MFALME WA ASSISTS

Barcelona playmaker Xavi ameshacheza Classico 30, akifunga mabao 4 na akitoa assists nane japokuwa katika hizo pasi za mwisho 8, nne kati hizo alizitoa katika mchezo waliofungwa Madrid 6-2 katika uwanja wa Bernebau in May 2009.


ZIDANE ZINEDINE


Kuafuatiwa na usajili wake uliovunja rekodi ya dunai baada ya Madrid kulipa €75 million kwa Juventus IN 2001. Zinedine Zidane alifunga katika mechi zake zote mbili za kwanza katika uwanja wa Santiago Bernebeu.

No comments:

Post a Comment