Search This Blog

Friday, March 16, 2012

WATU 75 WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA KESI YA VURUGU UWANJANI NCHINI MISRI

Nchini Misri huku familia mbalimbali zikiendelea kuomboleza vif via wapendwa wao waliopoteza maisha kwenye vurugu zilizozuka uwanjani katika Mchezo wa ligi kuu Kati ya national al ahly na al masry, watu 75 wamepandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kushiriki kwenye vurugu hizo.


Waliopandishwa kizimbani ni pamoja na maafisa tisa wa jeshi la polisi akiwemo mkuu wa jeshi Hilo meja jenerali Issam samakk. Kwa kujibu wa taarifa ya mwendesha mashtaka wa mahakama kuu nchini misri, vurugu zilizotokea siku ya mchezo zilipangwa kabla  na ushahidi wa kila mikanda ya televisheni unaonyesha baadhi ya mashabiki wakitumia silaha walizoingia nazo uwanjani wakiwa na malengo ya kuwadhuru mashabiki wa timu pinzani.


 Kwa upande wa washtakiwa ambao ni maafisa wa jeshi la polisi wanatuhumiwa kwa kushindwa kudhibiti hali iliyotokea huku wakijua kuwa baadhi ya mashabiki walikuwa na lengo la kuanzisha vurugu. 


 Nayo timu timu ya Al Masry ambayo mashabiki wake ndio walioanzisha vurugu hizo, inatarajiwa kupewa adhabu kali ambayo wengi wanaamini adhabu hiyo huenda ikawa ya kushushwa daraja huku uwanja wake ukifungiwa kutotumika kwa michezo yoyote ya kiushindani.

No comments:

Post a Comment