Search This Blog

Friday, March 9, 2012

WADAU NA MCHANGO WENU

Na Hassan Lemma

Wakati maximo anachukua timu ile nafasi ya 134 mnamo august 2006 imekua ikipanda nafasi kila kukicha tulikua katika wastani wa nafasi za tisini yaani tulikaribia nafasi ya 75 ammbayo ingemuwezesha mchezaji wetu kutoka ligi yetu na kwenda kucheza Premier League ya UK..mnamo december 2007 tulifikia kiwango ambacho sidhani kama tuliwahi kufikia huko nyuma yaani nafasi ya 89 lakini tulishuka kidogo miezi iliyofuata mpka ilipofika August 2009 tukifika nafasi ya 93 na nafasi mbaya aliyowahi kufika maximo ni miezi mitatu baada ya kuchukua timu ambayo ni nafasi 121 october 2006 ambayo bado nasema ni nzuri maana miezi miwili ya nyuma tulikua nafasi 134 lakini baada hapo kama ni nafasi ya juu aliyoshuka basi ili may 2007 na september 2008 yaani nafasi ya 117 basi majungu yakaan...za baadae tukashindwa kumuongezea mkataba sababu kubwa ikiwa ni kuwaacha baadhi ya wachezaji ambao yeye aliona hawana nidhamu na baadhi ya wachezaji hao wameonyesha kuwa hawana nidhamu hata baada ya kuteuliwa na makocha wazawa na huyu Jan Poulsen na nikianza na huyu kocha wa sasa Jan Poulsen amepewa timu ikiwa nafasi ya 111 katika rank za fifa lakini kila siku timu inashuka mpaka february hii tupo katika nafasi ya 139...yaani imepita hata wakati ule tukiwa na kocha wazawa wakina mshindo Msolwa kama sijakosea.....Maswali ni haya; 1. TFF inaturudisha kule tulikotoka kabla maximo hajapewa kazi??? 2. Kuna sababu gani ya kuendelea na Jan Poulsen kwa sasa au ni kipya gani anachokionyesha kwa sasa???? 3. Nini kazi ya Mkurugenzi wa Ufundi TFF???? 4. Je Mikoani hakuna wachezaji ambao wanafaa taifa ambao hawapo timu za ligi kuu 5. Je Mfuko wa rais unamlipa kocha haufanyi tathimini maana kuendelea kumlipa mtu ambae kazi yakae kukurudisha nyuma ni upuuzi 7. Wadhamini wa TAIFA STAR NMB na SERENGETI huu udhamini usio na tija mnaondelea nao kwa timu ya taifa unamanufaa kwenu binafsi lakini sio kwa watanzani ??na mengine mengi nitaendelea kuuliza baadae :
SULUHISHO
1.Kuna kila sababu ya watanzania kugomea kwenda kuangalia mazoezi ya timu ya taifa na mechi zake
2. Wadhamini kuvunja udhamini kwa Taifa star na kuidhamini Twiga Star

Ndugu mdau niambie unachofikiri maana hii ni makala ndefu nimeomba magazeti mengi niweze kuitoa hapo juu ni kama kasamari kadogo kwa makala yenyewe kuhusiana na Timu ya Taifa na TFF na pia hayo ni baadhi ya maswali tu machache na kila swali pia lina makala yake.....


.kwa mawasiliano zaidi hlemmeh@ yahoo.com

No comments:

Post a Comment