Search This Blog

Thursday, March 1, 2012

MOURINHO ASEMA: "SIRUDI CHELSEA"


Mourinho akiwa na shabiki nje ya mgahawa uliopo jijini London.


Kocha wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho amesema hatorudi  Stamford Bridge msimu ujao.
Zilipotoka picha za mreno huyo akiwa anatafuta nyumba mjini London baadhi ya watu wakachukulia kwamba boss huyo wa Real Madrid alikuwa akitafuta nyumba kwa jili ya kuweza kurudi mjini humo kuchukua nafasi AVB.
Lakini, according to Daily Mirror, Mourinho amemwambia mmiliki wa mgahawa anaoupenda mjini London kwamba harudi Chelsea.
Marrietta Maccioni, motto wa kike wa Alvaro Maccioni, mmiliki wa mgahawa wa La Famiglia, alisema: “ Ilikuwa vizuri sana kumuona tena hapa baada ya muda mrefu sana.
“Alikuja na mkewe, shemeji yake pamoja na mume wa shemeji yake. Walikula chakula cha mchana na kufurahia sana.
“Jose alikuwa akiongea na baba yangu kwa muda mrefu akamwambia anatafuta nyumba katika eneo hilo kwa ajili ya familia yake.
Enzi hizo.



“Watu wengi wakiwemo wafanyakazi wa Chelsea walikuwa wanauliza kama amesema anarudi Stamford Bridge lakini kwa bahati mbaya Jose alisema harudi Chelsea. Tumesikitika sana kwa sababu Mourinho ni kocha mzuri. Hakutuambia kitu kingine chochote kuhusu mipango yake ya baadae.”

No comments:

Post a Comment