Search This Blog

Thursday, March 1, 2012

DAVID LUIZ AMBWATUKIA LAMPARD - AMWAMBIA HANA TOFAUTI NA YOYOTE NDANI YA CHELSEA NA AFUATE ANACHOAMBIWA NA KOCHA.


Luiz amejiingiza katika ugomvi na kipenzi cha Chelsea Lampard.


David Luiz ameingilia ugomvi kati ya Andre  Villas Boas na Frank Lampard baada ya kiungo huyo wa Uingereza inabidi afuate yote anayoambiwa na asifikiri yeye yupo tofauti na mchezaji yoyote ndani klabu hiyo.
Lampard amekuwa hana furaha na idadi ya mechi alizocheza msimu na wiki iliyopita alikiri kwamba hana mahusiano mazuri na AVB.
Mlinzi David Luiz amemtetea Villas-Boas  akisema, “Hakuna anayepaswa kuwa baba au mtoto wa Fulani katika timu ya soka. Hakuna kupendelewa. Lampard anabidi amsikilize kocha anapotokea amri na maelekezo na kufuata anachoambiwa au kuagizwa kufanya.
“Hamna mchezaji anayepaswa kujua kwamba yeye ni mwajiriwa tu klabu.”
Taarifa zimezidi kuzagaa kuhusu hatma ya AVB ambaye wiki kwa mara ya kwanza amekiri anaweza kufukuzwa kazi.
AVB amekalia kuti bovu @Stamford Bridge.



Lakini mbrazil Luiz anasema Mreno huyo amekuwa akionewa, pamoja na Chelsea kuwa nafasi ya tano katika ligi, na wakiwa katika hatari ya kutolewa katika champions league.
“Msimu uliopita, kulikuwa kuna timu ambazo zilikuwa nafasi mbaya katika msimamo lakini hakuna aliyezungumza hilo. Ni rahisi sana kuongea kuhusu AVB, kwa sababu Chelsea ni timu kubwa ambayo siku zote inatafuta nafasi ya kwanza na inapotokea ikiwa ya 3 au ya nne ni inakuwa rahisi kumpa lawama kocha. Lakini Andre ni mtu tofauti ana kila kitu kama kocha, ni mtu sahihi kabisa kwa Chelsea ana ataipa mafanikio makubwa klabu hii.”

No comments:

Post a Comment