Search This Blog

Saturday, March 24, 2012

CRISTIANO RONALDO AFIKISHA MAGOLI 101 KWENYE LA LIGA- AVUNJA REKODI YA PUSKAS

 Cristiano Ronaldo amekuwa ndio mchezaji wa kwanza wa Real Madrid kufikisha magoli 101 kwenye La Liga chini ya mechi 115, kufuatia kufunga goli katika mechi ya usiku huu dhidi Real Sociedad.

Mreno huyo sasa ameweka rekodi mpya katika klabu hiyo baada ya kufikisha idadi hiyo ya magoli baada ya kucheza mechi 92 tu.

Rekodi ya mchezaji aliyefikisha magoli 100 ya La liga kwa haraka ilikuwa inashikiliwa na mchezaji wa zamani wa timu hiyo Ferenc Puskas ambaye yeye alicheza mechi 115 mpaka kufikisha idadi hiyo ya magoli 100.

Goli la leo la Ronaldo ni la 45 katika msimu kuifungia Real Madrid na 34 katika La liga akimfikia Lione Messi mwenye 34.

No comments:

Post a Comment